언어/스와힐리어 연구

제2부. 스와힐리어 구문연습(Kiswahili Excercise) - 11장. Somo la Kumi na Moja

africa club 2015. 3. 15. 21:27

22.

23.

제 11 장

① Somo la Kumi na Moja 

 

가. 1. 회화

1) 1.1 호텔에서

 

A : Nataka kupatia chumba chenye choo cha kuogea(=chumba cha kuogea)? : 나는 욕실 달린 방을 원합니다.

B : Nasikitika hakuna nafasi. : 죄송합니다만 방이 없는데요.

A : Tafadhali simama hapa, Nataka kwenda choo. : 여기에 잠시 서 주세요. 화장실에 가고 싶습니다.

B : Unataka choo ndogo au choo kubwa? Yaani mkojo au kinesi? : 작은  일을 보고 싶으세요,  큰 일을  보고 싶으세요? 다시 말해서 소변이에요, 대변이에요?

A :  Nataka choo kubwa lakini hakuna karatasi ya choo. : 대변을 보고 싶습니다만 화장지가 없네요.

B : Lazima utumie karatasi ya mezani. / Lazima utumie majani. : 탁자에 있는 종이를 이용해야만 해요. / 풀잎을 이용해야만 해요.

A : Unataka kunywa kinywaji gani? : 어떤 음료수를 원하세요?

B : Nataka maji ya kunywa, pombe (Tuska / Ndovu / Kilimanjaro), chupa ya maji na soda kinywaji. : 물, 맥주(터스카 / 은도브 / 킬리만자로), 생수와 소다를 원합니다.

A : Nataka kukaa siku moja, Una nafasi? / Una chumba? : 나는 이곳에서 하룻밤 묵고 싶습니다만 방 있어요? / 당신은 방을 가지고 있습니까?

B : Una watoto wangapi? : 아이가 몇 명이나 있어요?

A : Nini gharama ya kila siku moja? / Pesa ngapi kila siku moja? / Nauli ngapi kila siku moja? : 하룻밤 묵는데 얼마예요?

cf.) gharama(-) : 소비, 지출, 지불, 비용, 요금, 총액. cf.) -fanya / -toa gharama : 지출하다.

B : Shilingi ya elfu moja kila siku moja. : 하룻밤에 1000 실링입니다.

A : Nataka chumba chenye eyakandishana / kiyoyozi / kisafisha hewa. : 에어컨이 있는 방을 주세요.

B : Nauli ni ghali zaidi. : 비용이 아주 비싼데요.

A : Inanilazimu nifute jina lini?  : 언제 체크아웃 해야 합니까?

B : lazima ufute baada ya chakula cha mchana. : 점심 식사 후에 체크아웃 해야만 합니다.

A : Naweza kukusaidia nini? : 제가 당신을 위해 무엇을 도와드릴까요?

B : Tafadhali sitaki kuamshwa kesho asubuhi.  : 내일 아침에 깨우지 마세요.

A : Unaweza kunisaidia kidogo ? : 당신이 저 좀 도와주실 수 있나요?

B : Nataka kufua nguo yangu halafu nataka kuipiga pasi. : 내 옷을 세탁하고 다림질을 하야거든요.

A : Sitaki mbu. Umepiga bomba katika nyumba langu. Umetayarisha chandalua. : 저는 모기가 싫어요. 제 방에 모기약을 뿌려주시고 모기장을 쳐주세요.

B : Nitaamrisha kupiga bomba. : 모기약을 뿌리도록 말하겠습니다.

cf.) amrisha : v. 명령하다. amri(-, ma-) : 1. 명령, 분부. 2. 권한, 지배, 책임.

A : Tafadhali jaza fomu (kitabu cha hoteli) hii. : 이 서류(숙박부)를 작성해주세요.

B : Lazima niandikie (habari yo yote) anwani, nambari ya simu na kadhalika? : 주소, 전화번호 등을 다 써야 하나요?

 cf.) nyumba : 집. chumba : 방. kichumba : 조그만 방.

A : Nina haja. Wapi kichumba cha wanawake? : 아주 급한데요. 숙녀용 화장실이 어디에 있어요?

B : Gorofa ya tatu. : 3층입니다.

A : Unataka kukaa katika nyumba aina gani? : 어떤 종류의 방에 묵으시겠습니까?

B : Nataka chumba chenye kuelekea bahari? : 나는 바다를 향한 방을 원합니다.

A : Unacho kilicho, bora kuliko hiki? Au una chumba kizuri zaidi? : 이 방보다 더 좋은 방이 있습니까?

B : Kuna nafasi lakini ghali sana. : 있습니다만 값이 비쌉니다.

A : Nataka viatu hivi vipigwe rangi. / Unaweza kunipiga rangi viatu vyangu? : 구두를 닦고 싶은데요. 내 구두를 닦아 주실 수 있습니까?

B : Pesa ngapi utanilipia? : 당신은 나에게 얼마를 주시겠습니까?

A : Itachukwa tayari saa ngapi? : 몇 시에 준비가 될까요? / Ninahitaji kesho asubuhi mapema. : 나는 내일 아침 일찍 필요합니다.

B : Sawasawa. 좋습니다.

 

2) 1.2 레스토랑 / 카페에서

 

A : Pesa ngapi kwa jumla? : 모두 얼마예요?

B : Vitu vyote ni shilingi mia tano na sabini. : 모두 570 실링입니다.

A : Nina kiu. Nataka kunywa soda, mkahawa iko wapi? : 나는 아주 갈증이 납니다. 소다를 마시고 싶어요. 식당이 어디에 있습니까?

B : Iko karibu na posta. : 우체국 옆에 식당이 있습니다.

A : Niletee kisahani cha jivu  ashtray tafadhali! : 나에게 재떨이를 가져다 주시겠습니까?

B : Hiki hapa. : 여기 있습니다.

A : Unataka soda gani? : 어떤 소다(음료수)를 원하세요?

B : letea / niletee chupa ya maji tu. : (나에게)생수를 가져다주세요.

A : Vitu gani viko mezani? : 탁자에 어떤 것이 있습니까?

B : Kijiko cha chai, kitambaa, sahani na kisahani. : 찻숟가락, 휴지, 접시와 작은 접시들이 있습니다.

A : Letea gamba la kulia(vyakula) : 메뉴판을 가져다 주세요.

A : Nitaweza kula chakula cha asubuhi saa ngapi kesho asubuhi? : 내일 아침에는 몇 시에 아침 식사를 할 수 있습니까?

B : Nataka kuondoka kesho asubushi saa kumi na mbili mapema. Unaweza kutayarisha chakula cha asubuhi kabla ya kuondoka? : 나는 내일 아침 6시에 일찍 떠나고 싶습니다. 출발하기 전에 아침을 준비해주실 수 있나요?

A : Tupe meza karibu na dirisha. : 창문 옆에 있는 테이블을 주세요.

B : Karibu na dirisha imejaa. : 창가의 테이블은 다 찼어요.

A : Ukotayari kuagiza chakula? : 음식을 주문할 준비가 되었나요?

B : Ndiyo! Ningependa kuagiza chakula sasa. : 예! 나는 지금 음식을 주문하고 싶어요.

A : Umeshachagua chakula gani? : 음식을 선택하셨습니까?

cf.) chagua : v. 선택하다, 고르다.

B : Unaweza kutushauri(=sifia) nini? : 우리에게 무엇을 추천하시겠습니까?

cf.) shauri : 1. v. 추천하다, 권하다(=sifia). 2. (ma-) : 계획, 의도, 프로젝트, 충고, 상담. sifia / sifu : v. 찬양하다, 칭찬하다, 추천하다, 권장하다.

A : Nina chakula maalum leo. / Una chakula maalum? :  오늘의 특별요리는 무엇입니까?

B : Nataka kusifia chakula cha kienyeji. : 오늘은 전통요리를 추천하고 싶습니다.

A : Unataka kula chakula aina gani? : 어떤 종류의 음식을 원하세요?

B : Napenda chakula cha Kiasia. : 나는 아시아 음식을 좋아해요.

cf.) Asia : 아시아. mwaasia(wa-) : 아시아인

A :  Nina njaa sana. Tafadhali ongeza kidogo. : 조금 더 주세요!

B : Letea pesa zaidi. 돈을 더 내셔야 해요.

A : Nasikia njaa. Habari za chakula maalum leo? : 나는 배고파요. 오늘 어떤 음식이 특별합니까?

B : Vyakula vyo vyote ni tamu sana. : 모든 음식이 아주 맛있습니다.

A : Ulikula chakula cha Korea? : 한국음식을 먹었습니까?

B : Pilipili hoho kali sana. : 고추가 아주 메워요.

A : Unapenda kuagiza cho chote zaidi? : 더 주문하시겠습니까?

B : Ashante, nimeshiba : 고맙습니다만 나는 배불러요.

A : Tadhali niletee hesabu bill. : 계산서를 가져다 주세요.

B : Hii ni hesabu ya vyakula, hii ni hesabu ya vyniwaji. : 이것은 음식 계산서이고 이것은 음료수 계산서입니다.

A : Bakshishi ni katika hesabu hii? / Bakshishi iko ndani? : 팁도 이 계산서 안에 포함되어 있습니까?

cf.) bakshishi / bakhshishi(-) : 선물, 팁, 보상금, 기부금.

B : Ndiyo, iko katika bill yako. : 예, 당신의 영수증에 포함되었습니다.

A : Watu wa Korea wapenda kula chakula cha mchuzi na wali. : 한국 사람들이 고기 스프(고깃국)과 밥을 좋아합니까?

B : Kwa nini? : 왜요?

A : Kwa sababu majira ya kusini ni baridi sana katika Korea. : 왜냐하면 겨울에는 한국이 아주 춥거든요.

A : Ungependa kula chakula cha utamaduni katika Kenya? : 케냐에서 전통음식을 먹는 것을 좋아하세요?

B : Nyama ya kuchoma. Ni nzuri sana. : 야마초마가 아주 좋더군요.

A : Ungependa kula nyama ya kuchoma gani? : 어떤 야마초마를 좋아하세요?

B : Nyama ya n'gombe, nyama ya kondoo, nyama ya kuku, nyama ya ndama,  nyama ya ngruwe, nyama ya mbuzi. Lakini watu wa Korea wanataka kula nyama ya mbuzi. Kwa sababu nyama ya mbuzi ghali sana na mzuri kwa afya. : 소고기, 염소, 닭, 송아지, 돼지, 염소고기를 좋아해요. 그러나 한국 사람들은 염소고기를 좋아해요. 왜냐하면 염소고기는 아주 비싸고 건강에 좋기 때문이지요.

A : Ungependa kula chakula gani cha asubuhi? : 아침에는 어떤 음식을 좋아해요?

B : Kwa kawaida napenda kula tosi mbili na maziwa. : 일반적으로 토스트 2개와 우유를 좋아해요.

cf.) tosi(-) : 토스트

A : Je unataka chakula? : 음식을 원하세요?

B : Ndiyo bwana. Kuna chakula gani? : 예, 어떤 음식이 있어요?

A : Kuna matunda, keki, maandazi, na uji na mayai kadha wa kadha. : 과일, 케이크, 만다지, 우지, 계란 등이 있어요.

B : Tafadhali niletee kiazi. : 감자를 가져다 주세요.

A : Watoto wangu wana njaa. Mna chakula? : 아이들이 배가 고파요. 어떤 음식이 있어요?

B : Ndiyo, tuna matunda, mikate, chizi, saladi na omuleti kadha wa kadha. : 예, 과일, 빵, 치즈, 샐러드, 오믈렛 등이 있어요.

A : Tafadhali waletee jemu na mikate. : 그들에게 잼과 빵을 가져다주세요.

A : Yeye anakunywa gani? : 당신은 어떤 주스를 마실 겁니까?

B : Anakunywa juisi ya nyanya. : 토마토 주스를 마시겠습니다.

cf.) maji ya zabibu / nyanya : 포도 / 토마토 주스. maji ya matunda : 과일 주스

A : Una gani ya maji ya matuda? : 어떤 과일 주스가 있어요?

B : Nyingi sana. : 아주 많아요.

A : Una matunda aina gani? : 어떤 과일이 있어요?

B : ndizi, nazi, maembe, mapapai, chenza kadha wa kadha. : 바나나, 파인애플, 망고, 오렌지 등이 있어요.

cf.) chenza(ma-) : 첸자(오렌지의 일종)

3) 1.3 색(色)의 표현

Huu ni ukurasa. Ni rangi nyuepe.

Hili ni rinda. Ni rangi nyeupe.

Huu ni mpira. Ni rangi nyeupe.

Huu ni uzi. Ni rangi nyeusi.

Nili ni shati. Ni rangi nyeusi.

Huyu ni mbuzi. Ni rangi nyeusi.

Huu ni mkoba. Ni rangi nyekundu.

Huyu ni kuku. Ni rangi nyekundu.

Hili ni gari. Ni rangi nyekundu.

Hili ni shati. Ni rangi ya kijani.

Hii ni kofia. Ni rangi ya kijani.

Hiki ni kiatu. Ni rangi ya kijani.

<원문출처 : Mchangamwe, Aboud B., Msingi wa Kiswahili: Darasa la Kwanza (Nairobi, Longhorn Publishers Ltd., 2003), p. 31.>

 

4) 1.4 수수께끼(Kitendawili)

 

Mwalimu : Mwalimu, tafadhali nieleze sarufi ya sentensi hii.

Mwanafunzi : Huielewi?

Mwalimu : Ndiyo.

Mwanafunzi : Ulikuwa wapi nilipoieleza?

Mwalimu : Nisamehe; sikuwapo ulipoifundisha.

Mwalimu : Wakati anapotaka kutoa kitendawili, mtu husema nimi?

Mwanafunzi : Husema "Kitendawili!"

Mwalimu : Na wasikilizji husema nini?

Mwanafunzi : Wao husema "Tega!"

Mwalimu : Niambie Maana ya "kitendawili" kwa Kiingereza.

Mwanafunzi : Maanake ni “riddle” kwa Kiingereza.

<원문출처 : Hinnebusch, Thomas J. & Mirza, Sarah M., Kiswahili, 2nd edition (Washington, University Press of America, Inc., 1998), pp. 175.>

 

 

나. 2. 구문연습

1) 2.1 Wanapendeza

 

Angalia watu hawa wanavyopendeza. Kila mmoja amevaa vazi la kwao. Wanafanya mashindano ya mavazi. Msichana amevaa gauni na kanga. Pia amejifunga kilemba. Wavulana wamevaa mashati na suruali. Wengine wamevaa kanzu na kofia. Pia wapo waliovaa lubega. Chini wamevaa viatu na soksi. Wengine wamevaa kandambili. Nani atashinda? Sijui. Maana wote wanapendeza.

<원문출처 : Rashid, M.K., Kiswahili Darasa la Kwanza (Iringa, Baraka Publishers Limited, 2003), p. 72.>

2) 2.2 Popi

Mbwa wetu anaitwa Popi. Popi ni mweusi mwenye madoa meupe. Popi ana masikio marefu. Akikimbia masikio yake huchezacheza.

Popi ni mkali sana. Akimwona mgeni hubweka woo! woo! woo! Popi akimwona paka hulia woo! woo! woo! Baba humfunga kwa mnyororo. Anasema mbwa ni hatari. Anaweza kumuuma mtu.

Popi hupenda sana kula nyama. Ana meno mkali sana. Anapenda kutafuna mifupa. Anapenda kutafuna mifupa. Mimi ninampikia mbwa chakula chake kila siku.

Zamani Shani alikuwa hampendi Popi. Akimwona alikuwa anafutuka na kuunguruma ngrrru! Popi naye alikuwa akibweka na kukimbia. Siku hizi wanapendana. Sisi tunawapenda Popi na Shani. Na wao wanatupenda. Tunacheza nao kila siku. Cheka anampenda Shani tu. Anamwogopa Popi.

<원문출처 : Mbilinyi, Dorothy A.S., Kiswahili: Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Ben and Company Ltd., 2002), pp. 30-31.>

3) 2.3 Babu na Bibi

Mimi ninaitwa Baraka. Babu na bibi wanakaa na sisi nyumbani. Babu ni mzee sana. Hawezi kufanya kazi. Bibi anaweza kufanya kazi ndogo ndogo. Bibi akiamka asubuhi hufagia uwanja. Kisha huchoma moto takataka. Uwanja unakuwa safi sana.

Babu ni hodari sana wa kusimulia hadithi. Juzi alitusimulia kuhusu njaa kubwa iliyotokea zamani sana. Hapakuwa na chakula.

Wazazi walichemsha mawe. Watoto walikuwa wanasubiri mawe yaive. Mwisho wake wakalala. Sisi tunapenda sana hadithi.

Mara nyingi jioni bibi humenya mihogo au viazi. Siku nyingine anazunguka kwenye shamba letu kuokota kuni. Anazipanga kwenye kichanja nje ya nyumba yetu. Jioni anakoka moto nje. Mimi na rafiki zangu tunakuja kuota moto pamoja na bibi na babu.

<원문출처 : Mbilinyi, Dorothy A.S., Kiswahili: Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Ben and Company Ltd., 2002), pp. 36-37.>

 

4) 2.4 Rangi Mbalimbali

Kuna rangi za aina nyingi. Kuna rangi nyeupe, nyeusi na nyekundu. Rangi nyingine ni rangi ya kijani, manjano na bluu. Mimi ninapenda nguo zenye rangi ya bluu na nyeupe. Nguo zetu za shule zina rangi mbili. Rangi nyeupe na rangi ya bluu. Mama ana gauni la njano. Kanga zake ni za rangi nyekundu na nyeupe. Baba hupenda kuvaa shati la rangi nyeupe. Baba hupenda kuvaa shati la rangi nyeupe. Wakati mwingine huvaa shati la rangi ya kijani na suruali nyeusi.

Katika shule yetu, watoto wote huvaa mashati meupe. Wavulana huvaa kaptura ya bluu na wasichana huvaa sketi za rangi ya bluu. Nguo za shule zinapendeza sana. Mwalimu wetu hupenda sana kuvaa shati la rangi ya bluu na tai. Kila wakati anaonekana nadhifu sana.

Maua ya shule yetu ni ya rangi nyingi. Tumepanda maua mekundu na meupe. Mengine ni ya rangi ya manjano. Shule yetu inapendeza kuwa na maua ya aina mbalimbali. Kila siku asubuhi na jioni, wanafunzi wanamwagilia maji maua. Maua yasipomwagiliwa maji yatakauka. Sisi hatupendi kuona maua ya shule yetu yanakauka.

<원문출처 : Ndilime, D.M., Kiswahili 1: Shule za Msingi Tanzania :  Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Macmillan Aidan, 2002), p. 78.>

5) 2.5 Mchezaji soka na : wachezaji ngoma

 

Alison : Joseph ni mpwa wako?

Francis : Ndiyo, ni mwana wa dadangu. Kwa kawaida anacheza mpira Jumamosi.

John : Ni mchezaji soka katika timu ya ligi?

Francis : Ndiyo, na mimi ni mwanachama wa klabu yake! Alitarajia kucheza mechi ya kirafiki leo, siyo ya ligi. Imeahirishwa kwa sababu ya mvua nyingi usiku. Ameambiwa kwamba uwanja umejaa maji. Ni kama mafuriko huko. Hata hapa pana tope. Tusimame pale kando tujikinge tope.

Alison : Kumeanuka sasa.

Francis : Ndiyo. Mawingu hayaonekani. Kama mvua itanyesha tena tutatumia mwavuli wangu. Tazama, ni mkubwa kabisa!

Alison : Joseph yuko wapi? Simwoni sasa.

Francis : Yupo pale mlangoni. Anapiga soga tu. Harakisha bwana! Kiwanjani panajaa watazamaji. Tutafute viti karibu na jukwaa!

Joseph : Watacheza ile ngoma ya Kisukuma ya kutumia nyoka? Ni ngoma ya kupendeza sana.

Francis : Bila shaka wataicheza. Huweka kikapu jukwaani. Wakati wanapocheza, nyoka anaonekana kujitokeza.

Alison : Tutaona ngoma nyinginezo?

Francis : Hatutaona nyingine za kutumia nyoka. Nyingine zitakuwa za aina mbalimbali za kikabila. Moja ni ya Kinyakyusa, nyingine ni za Kibena, Kimeru, Kihaya na kadhalika. Katika ngoma wanazozicheza Wahaya, wachezaji huruka juu sana, kana kwamba ni ndege. Mtaona ngoma nyingi leo.

Alison : Inawezekana kutakuwa kumekuchwa kabla tamthilia haijaanza!

Francis : Inawezekana, lakini pana taa kubwa za umeme kwenye jukwaa, pale...na pale...mnaona? Aa! Rafiki yangu Augustine yupo palepale pembeni. Mnamwona mrefu yule? Ni meneja wa kikundi cha wachezaji. Tulisoma pamoja shuleni. Baadaye mtakutana naye. Michezo inaanza sasa hivi.

<원문출처 : Russell, J., Swahili (Abingdon, Teach Yourself Books, 1996), pp. 255-156.>

6) 2.6 Mashairi

 

Leo tusome mifano ya mashairi. Tutazame kwanza mfano wa shairi la mapenzi. Shairi hili liliandikwa na mshairi mtukufu, Bwana K. Amri Abedi. Bwana Abedi alikuwa Mswahili kutoka Unguja; aliandika mashairi mengi kuhusu mapenzi na dini. Mfano mmoja. jina lake niUkitaka Moyo Wangu, ni hili:

 

Ukitaka Moyo Wangu

Ukitaka moyo wangu, ni tayari kukupao

Nawe wako uwe kwangu, usiwe kwa mungineo

Hapa t'akufanya wangu, niwe wako wa pekeo

Mpumbavu apendao, pendo upande mmoja.

 

Shairi jingine la mapenzi ni hivi: (halina jina na hatujui mwandishi wake):

 

Mahaba ni sumu, ni sumu katili

Mahaba ni tamu, kwa watu wawili.

 

Mashairi hayo mawili ni mafupi sana. Lakini mashairi mengi ni marefu sana yenye mistari kama kumi na miwili hivi au zaidi. Mashairi mengi ni vigumu kusoma kwa ajili ya maneno mengi magumu ya zamani na ya Kiarabu. Katika mifano hiyo miwili kuna maneno machache sana ya Kiarabu (katili ni mfano mmoja) lakini sarufi ya shairi la kwanza ni ngumu kidogo. Kulingana na Kiswahili sanifu ni tofauti kidogo (tazama Msamiati mwisho wa somo hili kwa maelezo ya sarufi ngumu na maneno magumu).

Kwa kawaida mashairi hutungwa kufuata kanuni na sheria za mashairi. Shairi lisilofuata sheria na kanuni hizo huitwa guni. Mashairi hayo mawili yanafuata sheria. Tunaona katika la kwanza kwamba kila mstari una mizani sawa, yaani kila mstari una silabi kumi na sita, la pili lina silabi kumi na mbili kila mstari. Mizani ya mashairi hupimwa kwa silabi. Shairi la kwanza lina silabi kumi na sita; la pili lina kumi na mbili:

 

U-ki-ta-ka   mo-yo   wa-ngu   ni   ta-ya-ri   ku-ku-pa-o

1  2  3  4    5  6    7   8     9   10 11 12   13 14 15 16

Ma-ha-ba   ni   su-mu   ni   su-mu   ka-ti-li

1   2   3   4    5   6    7    8  9    10 11 12

 

Pia mashairi hayo yanafuata sheria za vina; kwa mfano katika shairi la pili, vina vya kati (vya silabi ya sita) na vya mwisho ni hivi: -a -b / -a -b.

Vina vya shairi la kwanza ni sawa na vina hivyo, ila mstari wa mwisho, na huo una kina tofauti, yaani: -a -b / -a -b / -a -b / -b -c.

Wakati washairi wanapoandika mashairi, wengi hufuata kanuni hizo; ijapokuwa hivyo wengi huandika guni. Zamani mashairi yaliandikwa kwa maandiko ya Kiarabu. Siku hizi washairi hutumia herufi za Kizungu (yaani za Kirumi).

<원문출처 : Hinnebusch, Thomas J. & Mirza, Sarah M., Kiswahili, 2nd edition (Washington, University Press of America, Inc., 1998), pp. 176-178.>

7) 2.7 Familia na ukoo

Mifumo ya Kiafrika ya koo, ndoa, na uzaaji wa watoto ni mambo ya kuvutia kwakuwa ni tofauti na jinsi watu wengi wanavyodhani inapaswa kuwa. Wasafiri wengi barani Afrika wamekuwa wakimpa mtoto kitu cha kula katika jiji fulani la Kiafrika, kisha kumuona mtoto huyo akiwageukia wenzake na kula nao pamoja kitu hicho alichopewa. Hali hii inatokana na tofauti ya utamaduni unaotumika kulelea watoto.   

Watoto wa Kiafrika hufunzwa kadri wanavyokua, kushirikiana; na aina hii ya ushirikiano haienei tu miongoni mwa watoto, bali pia kwa jamii nzima ya Kiafrika. Eneo lingine linalowavutia wasafiri wanaotembelea barani Afrika ni jinsi suala la ndoa na ukoo linavyoratibiwa. Sababu nyingine kwanini suala la ukoo barani Afrika huratibiwa hivyo ni kwamba wakati wanapozungumzia kuhusu familia, kama wazungu wanavyofanya, wanaonekana kujali zaidi jambo fulani tofauti na msisitizo wa kawaida wa familia ndogo. Hivyo, suala la ukoo linavutia sana.

Tofauti kuu kati ya mifumo ya koo ya Kiafrika na Ulaya-Amerika ni msisitizo unaowekwa barani Afrika kwa watu wanaojiona ni ndugu wa damu. Koo za Kiafrika hujumuisha hata makundi mengine wakati koo za kizungu huundwa na ndoa. Hali hii huzifanya koo za Kiafrika kuwa eneo changamani la utafiti. Aina zote mbili za ndoa kuanzia ile ya mitala-jike, ambapo mwanamke mmoja huolewa na kijiji kizima (mke mmoja, wanaume wengi) na mitala-dume (mwanaume mmoja huoa wanawake zaidi ya mmoja) ni mifano ya aina za ndoa zilizopo barani Afrika, hivyo kufanya ndoa kuwa jambo muhimu katika kuwaunganisha ndugu.     

Lengo kuu la ndoa barani Afrika ni kuzalisha watoto. Japokuwa familia na koo zilikuwa ni mifumo imara, wakati huu zinakabiliwa na changamoto mbalimbali. Miongoni mwake ni ukoloni na nguvu za kijamii zilizozuka baada ya ukoloni kama vile utandawazi. Wakoloni katika nchi za Afrika walipandikiza tamaduni zao katika jamii za Kiafrika hivyo kuathiri baadhi ya masuala ya kitamaduni kama vile ndoa na koo. Ukristu ni changamoto nyingine kuu kwa miundo ya Kiafrika kwakuwa mafundisho yake mengi yanapinga desturi za Kiafrika kama vile mitala.

Uhamiaji mijini ni changamoto pia, kwakuwa watu wamekuwa wakihamia mijini, familia kuvunjika hivyo kuwa ngumu kudumisha misingi ya koo. Hali hii inaleta changamoto nyingine ya UKIMWI kwakuwa watu hulundikana mijini ambako kuna ukosefu wa ajira, hivyo kuwalazimisha wanawake kugeukia umalaya kuwa ndiyo njia yao kuu ya kujipatia kipato. Pamoja na changamoto hizi, Waafrika wanaendelea kudumisha misingi ya koo japokuwa si kiumadhubuti kama ilivyokuwa hapo awali.   

<원문출처 : 아래의 내용을 요약하여 스와힐리어로 번역하였음. Gordon, April. A. & Gordon, Donald. L., Understanding Contemporary Africa (Boulder & London, Lynne Rienner Publishers, 2006), pp. 265-291(Family and Kinship).

다. 3. 문법

1) 3.1 관계대명사 vyo의 용법

 

관계 대명사 vyo는 '방법(manner, how, the way, the extent of some occurrence)'을 나타내기 위해 사용된다. vyo는 kama(~처럼 ; like, as, if 등), namna(방법 ; how, sort, kind, type 등)와 함께 사용된다.

 

(1) Mfano)

(2) Fanya (kama) ninavyosema; usifanye (kama) ninavyotenda. : 내가 말한 것처럼 해라. 내가 행동한 것처럼 하지 마라.(Do as I say; not as I behave.)

(3) Andika namna alivyosema. : 그녀가 말한 것처럼 써라.(Write how / the way she said.)

(4) Sujui jinsi, walivyounda jahazi lile. : 나는 그들이 어떻게 자하지(jahazi)라는 배를 만드는지 모른다.

(5) Soma kadiri uwezavyo. : 네가 할 수 있는 만큼 열심히 공부해라.

(6) Ni kama alivyosema, lugha ya Kiswahili ni umuhimu sana. : 내가 그에게 말했던 것처럼 스와힐리어는 정말 중요하다.

(7) Sipendi namna alivyoshona shati hili. : 나는 그녀가 이 셔츠를 바느질 한 것에 대해 좋아하지 않는다.

(8) Fanya kama upendavyo. : 네가 원하는 대로 하라.

 

3.2 관계접사가 사용된 지시사의 용법

'na(가지고 있다, have) 동사가 사용되는 문장에서는 명사에 상응하는 부류의 관계대명사를 붙여 표현할 수 있다. 이 경우에는 대명사 기능을 하거나 명확성을 더 나타내는 문장이 된다.

(9)

(10) Mfano)

(11) A : Una kitabu? : 너는 책을 가지고 있니?

(12) B : Sinacho. : 나는 그것을 가지고 있지 않아.

(13) A : Una watoto wangapi? : 당신은 아이가 몇 명입니까?

(14) B : Ninao wawili. : 두 명입니다.

(15) A : Una ndizi? : 당신은 바나나를 가지고 있습니까?

(16) B : Ninazo. : 나는 몇 개 가지고 있습니다.(명사나 명사구의 위치에서 대명사로서 기능)

(17) A : Wana vitabu vya Kiswahili? : 그들은 스와힐리 책을 가지고 있습니까?

(18) B : Wanavyo. : 그들은  몇 권 가지고 있습니다.(명사나 명사구의 위치에서 대명사로서 기능)

(19) A : Unazo ndizi? : 당신은 바나나를 가지고 있습니까?(명확성을 표시)

(20) B : Ninazo. : 나는 그것들을 가지고 있습니다.

(21) A : Wanavyo vitabu vya Kiswahili? : 그들은 스와힐리 책들을 가지고 있습니까?(명확성을 표시)

(22) B : Wanavyo. : 그들은 그것들을 가지고 있습니다.

(23) Mwalimu alikwenda nacho. : 선생님은 그것을 가지고 가셨다.

(24) Ninacho. : 나는 그것을 가지고 있다

(25) Tunazo. : 우리는 그것들은 가지고 있다.

 

명사 목적어와 함께 쓰일 때 명사를 한정하거나 특별한 것으로 표시한다. 다음에 나오는 문장들을 비교하여 보라.

(26)

(27) Mfano)

(28) Ninaona kitabu. : 나는 책을 보고 있다.(I see a/the book).

(29) Nina kitabu. : 나는 책을 가지고 있다.(I have a/the book.)

(30) Ninakiona kitabu. : 나는 그 책을 본다.(I see the book.)

(31) Ninacho kitabu. : 나는 그 책을 가지고 있다.(I have the book.)

영어에서는 지시사가 2개인데 비해 스와힐리어에서는 3개의 지시사가 있다. 이미 기술한 2개의 지시사는 영어의 지시 기능과 매우 흡사하다. 그러나 지금 설명하고 있는 지시사의 기능은 앞에서 언급된 것들을 설명하고 있기 때문에 “전술(前述)한 지시사(aforementioned demonstrative)라고 불린다.

(32)

(33) Mfano)

(34) kitabu hiki : 이 책(말하는 사람 가까이에 있을 때)

(35) kitabu hicho : 저 책(듣는 사람 가까이 있을 때)

(36) kitabu kile : 저 책(두 사람 모두에게 멀리 있을 때)

(37) Desturi kama hizo hazipatikani hapa. : 그것들(앞서 언급된)과 같은 관습은 여기서는 발견되지 않는다.(문단에서 이미 언급한 명사를 지칭할 때)

(38) Unataka kitabu kipi? : 어떤 책을 원하세요?

(39) Ninataka hicho. : (당신 가까이에 있는) 저것이요.(말하는 이보다 듣는 이에게 가까운 어떤 대상을 가리킬 때)

2) 3.3 na의 강조용법

 

na + 관계접사의 형태로 앞에 오는 명사를 강조할 수 있다. 아래의 첫 번 째 문장에서 비록 이 문장의 뜻은 글자 그대로 해석하면 '그 주제, 그리고 그것은 여행(The topic and it is tourism)'이지만, 이 문장에서 nayo의 기능은 mada를 강조하는 역할을 한다. 아울러 '또한(too, also, as well)'이라는 뜻으로도 쓰일 수 있다.

 

(1) Mfano)

(2) Mada nayo ni utalii. : 주제(강조)는 여행이다.

(3) cf.) mada(-) : 주제, 토픽.

(4) Watalii nao walimpa dereva zawadi. : 그 여행객들(강조)은 운전사에게 선물을 주었다. / 그 여행객들도 운전사에게 선물을 주었다.

(5) Mwalimu naye alikwenda nao. : 그 선생님(강조)이 그들과 함께 갔다. / 선생님도 그들과 함께 갔다.

 

만약 가상법이 사용된 동사 앞에 na가 사용될 경우 행동을 강조하는 의미를 나타낸다.

(6)

(7) Mfano)

(8) Basi, bila kupoteza wakati na tuanze. : 좋아, 시간을 허비하지 말고 (우리)시작하자.

(9)  

라. 4. 단어 및 어휘 정리

 

Asia : 아시아

bweka : v. 짓다.

choma : 불을 지르다, 굽다, 태우다.

fagia : v. 청소하다.

funga : v. 물다.

fupa(mi-) : 뼈.

futua : v. 꺼내다, 드러내다.

futuka : v. 1. 쥐어뜯다. 2. 폭로되다.

gauni(ma-) : 원피스, 긴 겉옷.

husu : v. ~ 에 관계하다, ~에 속하다, 나누어 주다. cf.) husiana : v. 서로 관련되다.

kandambili(-) : 샌들.

kichanja(vi-) / chanja(-) : 바구니 세공. cf.) chanja : v. 조각내다, 썰다.

kilemba(vi-) : 1. 터번. 2. 칭찬, 아첨.

kofia(-) : 모자.

kwao : ku+ao의 형태로 ‘그들이 사는 곳’이라는 뜻.

lubega(-) : 겨드랑이와 반대편 어깨를 두르면서 옷입는 방법.

maana(-) : 의미, 중요함.

menya : v. (껍질) 벗기다, 벗기다.

mnyororo / mnyoo(mi-) : 체인, 사슬, 차꼬. cf.) kamba(-) : 끈, 줄.

mwaasia(wa-) : 아시아인.

okoa : v. 구출하다, 구하다.

okota : v. 수집하다, 찾아내다.

ota : v. 1. 앉다, 털썩 앉다. 2. (손톱, 머리카락) 자라다. 2. 꿈꾸다.

panga : v. 정리하다.

shinda : v. ~보다 우수하다.

shindano(ma-) : 경기. cf.) shindano la mpira : 축구경기.

soksi(-) : 양말.

sumulia / simulia : v. 이야기하다, 설명하다.

suruali(-) : 바지. cf.) suruali fupi / kipande : 반바지. suruali ndefu : 긴바지.

tafuna : v. 씹다, 먹다.

uma : v. 1. 물다. cf.) Njaa inamwuma. : 그는 대단히 배가 고프다.(허기가 그를 물었다.) 2. 해치다, 아프게 하다. 3. 쏘다.

unguruma : v. 덜컥거리다, 천둥소리를 내다.

 

<속담>

●Kiwi cha yule, ni chema cha yule ; hata ulimwengu wishe. : 한 사람에게는 나쁜 일이 다른 사람에게는 좋은 일이 될 수 있다.

●Kilo sumu kwako ni dawa kwa mwenzio. : 너에게는 독인 것이 너의 상대에게는 약이 될 수 있다.

●Dhoruba ilipo, shwari ipo. : 폭풍우가 있는 곳에 고요함도 있다.

●Mla raha na uchungu hula. : 행복을 맛보는 자는 슬픔도 맛보게 된다.

●Hakuna kirefu kisicho mwisho. : 긴 역경도 마침내는 끝나게 되어 있다.

 

항상 자신이 처한 상황이 좋지 않더라도 또 설혹 아주 좋더라도 그러한 일은 언제든지 바뀌어 일어날 수 있다는 것을 가르쳐 주고 있다. 나아가 너에게는 의미 없고 쓸데없는 것 혹은 오히려 나쁜 일이 다른 사람에게는 좋은 것일 수도 있다는 것을 말해줌으로써 타인의 입장을 고려하라는 의미를 담고 있다.