언어/스와힐리어 연구

제2부. 스와힐리어 구문연습(Kiswahili Excercise) - 14장. Somo la Kumi na Nne

africa club 2015. 3. 15. 21:32

30.

31.  

제 14 장

① Somo la Kumi na Nne

 

가. 1. 회화

1) 1.1 환자의 질문

Nipatie daktari tafadhali? : 제가 의사선생님을 볼 수 있을까요?

Nahitaji daktari, haraka. : 나는 의사가 급히 필요합니다.

Daktari ataweza kuja kuniangalia hapa? : 의사가 저를 보러 오실 수 있나요?

Wakatii gani daktari ataweza kuja? : 몇 시에 의사가 오실 수 있어요?

Tafadhali mwite daktari. : 의사를 불러주세요.

Hospitali ya karibu iko wapi? / Unafahamu hospitali iliyo karibu? : 가까운 병원이 어디에 있습니까?

Tafadhali mwite muunguzi / askari polisi / gari la wagonjwa : 간호원 / 경찰 / 앰블런스를 불러주세요.

Amezimia. : 그는 기절했습니다.

Amejikata. : 그는 상처를 입었습니다.

Amechubuka. : 그는 타박상을 입었습니다.

Amevunjika. : 그는 골절되었습니다.

Ameteguka. : 그는 삐었습니다.

Nataka upigwe ekserei. : 나는 엑스레이 사진을 찍어보고 싶습니다.

Lazima niende kwa daktari. : 나는 의사에게 가보아야만 합니다.

Nataka kwenda kwa daktari. : 나는 의사에게 가보고 싶습니다.

Naweza kumwona daktari---kwa haraka? : 급하게 의사를 볼 수 있을까요?

Tangu siku kadhaa sijikikii vizuri. : 며칠 전부터 몸이 불편합니다.

Utaweza kunipa kitu cha kunipunguzia maumivu? : 통증을 덜어주는 것을 저에게 주실 수 있습니까?

Lini nitumie dawa? : 언제 약을 복용해야만 합니까?

Asante, nimepata nafuu kidogo. lakini bado sijawa mzima. : 덕분에 조금 나아졌습니다만 아직 완쾌되지는 않았습니다.

Niandikie cheti cha / kwa dawa hizi, tafadhali? : 처방을 해 주시겠습니까?

Nipatie risitii kwa ajili ya bima yangu, tafadhali? : 건강보험영수증을 받을 수 있을까요?

Tafadhali jaza fomu hii ya bima? : 건강보험서류를 작성해주시겠어요?

2) 1.2 의사의 질문

Unaumwa wapi? : 어디가 아프세요?

Umejeruhiwa? : 상처를 입으셨습니까?

Usijiongee. / Usidongee. : 움직이지 마세요.

Unaumwa wapi? : 어디가 아프세요?

Wapi panauma? : 어디를 다쳤어요?

Unapata maumivu ya namna gani? : 어떤 종류의 고통이지요?

Nitakupatia dawa za kupunguza maumivu. : 내가 진통제를 드릴게요.  

Unapata matibabu gani? : 어떤 치료를 받았어요? cf.) matibabu : pl. 의학적 치료 / 처치.

Unatumia dawa gani? : 어떤 약을 복용하셨어요?

Kwa muda gani unajisikia hali hii? : 얼마나 오랫동안 이런 상태였어요?

Hii ni mara ya kwanza kuwa hali hii? : 이런 경우가 처음이예요?

Nitakupima homa / presha. : 열 / 혈압을 재보겠습니다.

Tafadhali vua nguo mpaka kiunoni. : 가슴까지 옷을 올려주세요.

Fungua mdomo. : 입을 열어 주세요.

Vuta pumzi kwa nguvu. : 숨을 크게 들이쉬세요.

Kohowa, Tafadhali. : 기침을 해 보세요.

Umepata homa ya mafua. : 감기에 걸렸군요.

Nataka uende hospitali ukapimwe kila kitu. : 나는 검사를 위해 당신을 병원에 보내겠습니다.

Nataka uangaliwe na daktari maalumu wa magonjwa haya. : 나는 당신을 전문의에게 보내겠습니다.

<관련어휘>

bandeji / gongo(ma-) : 붕대.

bega(ma-) : 어깨부분, 견부.

chachi / shashi : 가제, (얇고 흰) 옥양목. cf.) karatasi ya shashi : 화장지.

chubuko(ma-) : 타박상, 좌상(挫傷).

daktari(ma-) / mganga(wa-) / tabibu(ma-) / ntabibu(ma-) : 의사.

damu(-) : 혈액, 피.

ependiks : 맹장염.

gari la wagonjwa : 구급차, 앰블런스.

homa ya mafua : 유행성 감기.

homa ya manjano : 황열.

homa(-) : 열병.

hospitali ndogo / zahanati(-) / dispensari(-) / kliniki(-) : 의무실, 진료소, 보건소.

huduma ya kwanza / msaada wa kwanza : 응급조치, 긴급처치. cf.) huduma / hoduma(-) : 봉사, 친절, 배려, 도움, 고용.

jeraha(ma-) : 부상.

kichocho(vi-) : 주혈흡충증.

kidole cha mkono : 손가락. kidole(vi-) : 손가락, 발가락.

kidole gumba : 엄지 손가락. cf.) gumba : adj. 1. 고독한, 고립된. 2. 아이가 없는, 불임의.

kipindupindu : 콜레라.

kisonono / kisunono(vi-) : 임질. cf.) kisonono cha damu : 주혈흡충증.

kitanda cha wagonjwa / machela(-) : 1. 들것. 2. 해먹.

kiungo(vi-) / kifungdo(vi-) : 관절.

kivi / kiko(vi-) : 팔꿈치.

kiwiko cha mguu : 발목. cf.) kiwiko(vi-) : 손목, 발목.

kobole(vi-) : 맹장(盲腸).

kope(ma-) : 눈꺼풀.

kuhara / harisho(ma-) / choo cha majimaji : 설사.  cf.) hara : 1.v. 변이 잘 통하게 하다, 설사하다. -hara damu : 이질에 걸리다. 2. (-) : (도시의) 지역, 지구.

kupigwa wa jua : 일사병.

kutoka damu : 출혈.

kuunguza : 화상. cf.) ungua : v. 타다, 겉을 태우다. unguza : v. 그슬리다, 타게 하다.

kuzimia : 기절. cf.) zimia : v. 기절하다, 까무라치다.

malale(-) / ugonjwa wakusinzia ugonjwa wa malale : 수면병. cf.) malale(-) : 수면병, 뇌염.

malaria(-) : 말라리아. cf.) homa ya malaria : 말라리아 열.

matako : pl. 엉덩이, 둔부.

matibabu : pl. 치료, 진료.

maumivu ya kichwa : 두통. cf.) umivu(maumivu) : 고통, 통증, 아픔, 쓰림.

mfupa(m-) : 뼈.

moyo(mioyo) : 심장.

Msalaba Mwekundu. : 적십자(赤十字).

mshipa wa damu : 혈관. cf.) mshipa(mi-) : 1. 정맥, 동맥. 2. 맥박. 3. 신경, 근육, 힘줄.

mshtuko / mstuko(mi-) : 1. 갑작스럽게 놀람, 발작. 2. 충격, 타격. 3. 삠, 겹질림. cf.) mshtuko wa ubongo : 졸도.

mvunjiko wa mfupa : 골절.

mwuguzi(wa-) : 간호원.

mzio(-) / wenga(-) : 알레르기.

nena(ma-) : 겨드랑이.

picha ya eksrei : 엑스레이 사진.

pima : v. 1. 재다, 측정하다. 2. 비판적으로 고려하다, 평가하다, 비판하다. cf.) -pima upana : 넓이를 재다. -pima halijoto la mwili : 체온을 재다. Halijoto ya kawaida ya mwili wa binadamu ni nyuzi joto 36.9'. : 일반적으로 사람의 몸의 온도는 36.9도이다.

risiti(-) / cheti(vy-) : 처방. cf.) risiti(-) : 수령, 수취.

shavu(ma-) : 뺨, 볼.

tiba / tabibia(-) : 약, 제약, 의약품.

ugonjwa wa kuambukiza : 전염병. cf.) ambukiza : v. 병을 옮기다, 유행시키다. ambukizo(ma-) : 병의 전염.

ugonjwa wa matumbo : 위염.

umedhurika na chakula kibaya : 식중독.

utunzaji / utunzi : sing. 간호, 보호, 돌봄.

3) 1.3 약국에서

Kuna duka la madawa karibu na hapa? : 이 근처에 약국이 있습니까?

Unayo dawa ya namna hii? : 이런 종류의 약이 있습니까?

Tafadhali nipe tembe ya aspirini. : 아스피린 정을 주십시오.

Tafadhali nipe dawa ya kuzuia homa. : 해열제를 주십시오.

Meza matone kumi ya dawa hii kabla ya chakula, mara tatu kila siku. : 1일 3회 식전에 이 약을 10방울을 복용하십시오.

Meza kidonge kimoja kabla ya kwenda kulala. : 주무시기 전에 1정을 복용하세요.

Zinanidhuru baadhi ya dawa za penisilin. : 나는 페니실린에 대해 부작용이 있어요.

Sitaki dawa iliyo kali sana. : 나는 너무 강하게 하고 싶지 않아요.

Nitumie kutwa mara ngapi? : 하루에 몇 번을 복용하는 것입니까?

<관련어휘>

bandeji / kitambaa cha kufungia : 붕대.

dawa ya kuharisha : 하제(下劑).

dawa ya kupakaa / makuru(-) : 연고, 고약.

dawa za kupata usingizi : 수면제.

dawa za kutuliza hali : 안정제.

dawa za malaria : 말라리아 약.

dawa(-, ma-) : 약, 치료.

kidonge(vi-) / kibonge(vi-) / tembe ya dawa : 정제, 알약, 정(錠). cf.) tembe(-) : 투약, 조제, 알약.

4) 1.4 몸이 아플 때

 

Bob anamtembelea Mkude nyumbani kwake; anamkuta amelala kitandani.

 

Bob : Vipi, Mkude bado umelala mpaka sasa?

Mkude : Ndiyo. Sijisikii vizuri. Tangu jana usiku nilikuwa mgonjwa.

Bob : Unasumbuliwa na nini?

Mkude : Ninaumwa kichwa na tumbo. Mwili wote unaniuma.

Bob : Umekunywa chai?

Mkude : Nimeshindwa kunywa chai. Ninajisikia kichefuchefu.

Bob : Basi hebu nikupeleke zahanati umwone daktari. Utakapomwona atakushauri.

Mkude : Sina nguvu kabisa. Ninaposimama miguu inatetemeka. Ninajisikia kizunguzungu.

Bob : Ngoja nikupeleke zahanati.

<원문출처 : Marshal, C. et. al., Sema Kiswahili : Furahia Tanzania, Version Two, A Kiswahili course for peace Corps Tanzania (Arusha, Peace Corps Tanzania, 1998), pp. 100-101.>

 

밥은 음쿠데의 집을 방문하여 그가 자고 있다는 것을 알게 된다.

 

밥 : 이봐, 음쿠데(Mkude) 지금까지 아직도 자고 있는 거야?

음쿠데 : 응. 나는 몸이 안 좋아. 어제 밤에 나는 아팠어.

밥 : 어디가 아픈 거야?

음쿠데 : 나는 머리와 배가 아파. 몸 전체가 아프다.

밥 : 차 마셨니?

음쿠데 : 나는 차를 마실 수가 없어. 나는 매스꺼워.

밥 : 내가 진찰을 받을 수 있도록 의사에게 데려갈게. 의사가 너를 진찰해 줄 거야.

음쿠데 : 나는 힘이 없다. 일어서려고 하면 다리가 후들거린다. 현기증이 나.

밥 : 기다려 내가 너를 병원에 데려갈께.

 

5) 1.5 병원에서 1

 

Daktari : Hali yako?

Mkude : Nzuri kidogo. Ninaumwa kichwa na tumbo.

Daktari : Umeanza kuumwa lini?

Mkude : Nilianza kuumwa tangu jana usiku.

Daktari : Muuguzi, tafadhali mpime homa. Kisha mwelekeze aende maabara apimwe choo, mkojo na damu. Baada ya kupimwa tutajua unaumwa nini na utapata matibabu.

Mkude : Asante.

Daktari : Usiwe na wasiwasi. utakapotumia dawa utakuwa mzima.

<원문출처 : Marshal, C. et. al., Sema Kiswahili : Furahia Tanzania, Version Two, A Kiswahili course for peace Corps Tanzania (Arusha, Peace Corps Tanzania, 1998), p. 101.>

 

<관련어휘>

bado : adv. 아직도, 여전히.

basi : cong. 1.(문장 첫머리에서) 자, 그때, 그래서, 그러므로, 그리고 나서 등. 2. (감동사로서) 일반적으로 동의, 수용을 표시한다. 그것으로 되었다. 알았다. 좋다 등. 3.(명령, 결정의 뜻) 거기까지! 이만 끝! 그만 두어라! 등 cf.) Basi twende! : 자아, 나가자!

daktari(ma-) : (서양)의사.

dawa(-, ma-) : 약, 치료.

hebu : interj. 여보세요! 잠깐! cf.) Hebu njoo! : 야, 잠깐 오너라!

hospitali(-) : 병원.

jana : 1.(-)과거, 이전. 2.adv. 어제.

kabisa : adv. 1. 완전히, 전체적으로, 모두. 2. 아주, 대단히, 극히. 3. 완벽하게, 정확히.

kichefuchefu : sing. 구역질, 매스꺼움.

kichwa(vi-) : 1.머리, 앞, 사물의 처음 ; 자랑, 거만함. 2. 윗부분, 주요 부분. 3. 주요 인물, 지도자. 4. adv. kichwa kichwa : 무모하게, 앞뒤를 가리지 않고. 5. 두통.

kitanda(vi-) : 침대.

kizunguzungu : sing. 현기증, 어질어질 함, 편찮음.

kozi(-) : 1. 코코넛의 섬유질, 2. 진로, 진행.

kunywa : v. 마시다.

kuta : v. 생기다, 일어나다, 우연히 만나다, 알게 되다.

kuwa : conj. 1. ya kuwa : ~하기 위하여, ~할 목적으로. 2. kwa kuwa : 왜냐하면. 3. v. 1. ~이다. 4. kuwa na : ~을 갖는다.

lala : v. 눕다, 자다.

mgonjwa(wa-) : 환자.

mguu(mi-) : 다리.

moyo(mioyo) : 심장, 마음.

mpaka sasa : 지금까지.

mwili(miili) : 1.(인간 혹은 동물의) 신체. 2. 머리를 제외한 몸통. 3. fig. 비행, (비행기의) 동체, 기체.

na : 1.(접속사로서) 그리고, ~과. 2.(전치사로서) ~와, ~으로, ~와 더불어, ~로부터.  3.(동사로서) 가지고 있다.

ngoja : v. 기다리다.

nguvu(-) : 1. 힘, 원기, 권력, 에너지. 2.권력, 능력, 영향력. 3. 중요성, 진지함. 4. 정렬, 격렬함, 맹렬함, 열성. cf.) kwa nguvu : 1. 힘차게, 강하게, 진지하게, 2, 강제로, 강압적으로, 마지못해서.

nini : interrog. pron. 무엇?

nyumba(-) : 집.

ona : v. 보다.

peleke : v. 데려가다, 인도하다.

shauri(ma-) : 1. 계획, 의도, 프로젝트, 안건.  2. 충고, 상담, 의논, 토의. 3. 토론, 논쟁. cf.) -fanya shauri : 고려하다, 의논하다, 기획하다.

shinda : v. 극복하다, 정복하다.

sikia : v. 1. 느끼다, 인지하다, 알다. 2. 듣다.

simama : v. 일어서다.

sindano(-) : 바늘, 주사.

sumbua : v. 걱정하다, 고민하다. cf.) sumbuliwa : v. 괴롭힘을 당하다.

tangu : prep. (=taka, kutoka) ~이래로, ~로부터.

tembelea : v. 방문하다. cf.) tembea : v. 걷다, 여행하다.  

tetemeka : v. 시시나무 떨듯 떨다. cf.) tetema : v. 떨다, 전율하다, 흔들리다.

tetemeko / tetemo(ma-) : 떨림, 흔들림, 전율, 진동.

tumbo(-) : 1. 배, 위. 2. 자궁. 3. 위장이나 내장의 통증. 4.fig. 어떤 물건의 내부. 5. 용기, 돌출.

umwa : v. 해를 입다. cf.) uma : v. 물다, 해치다, 아프게 하다.

usiku(siku) : 1.(siku) 밤, 야간(저녁 6시에서 아침 6시까지). 2. adv. 밤에.

vipi : interrog. 잘 지내? 어때? 이봐.

vizuri : adv. 좋은.

zahanati(-) : 의무실, 의료원.

6)

7) 1.6 병원에서 2

 

Juma : Shikamoo, Bwana Daktari.

Daktari : Marahaba Juma. Umefanya nini gotini?

Juma : Nilianguka na baiskeli.

Daktari : Pole, Juma. Hii ni jeraha kubwa. Mwuguzi Bi. Fatuma atakupaka dawa.

Mwuguzi : Hili jeraha linatoka damu. Ninavaa glavu zangu kwanza. Nitakupaka dawa. Kishaaa nitakufunga bendeji. Dawa inawasha. Usilie.

Juma : Loo! Dawa inawasha sana.

Mwuguzi : Usifungue hii bendeji. Rudi hapa baada ya wiki moja.

Juma : Ahsante sana. Kwahei.

Mwuguzi : Kwaheri ya kuonana.

<원문출처 : Marshal, Mchangamwe, Aboud B. & Jamaadar, A., Msingi wa Kiswahili 2: Darasa la Pili (Nairobi, Longhorn Publishers Ltd., 2003). ), p. 99.>

 

8) 1.7 에이즈에 관한 대화

 

Juma : Ukimwi ni ugonjwa hatari. Yapasa ujihadhari!

Muzi : Ndiyo, Ukimwi hauna dawa.

Juma : Mwenye Ukimwi akikuangalia, nawe umwangalie, Ukimwi utakushika.

Muzi : Kweli?

Juma : Mtu mwenye Ukimwi akikusalimia 'Habari yako' Ujibu, 'Nzuri‘ utakuwa umeshapata Ukimwi.

Muzi : Lo!

Juma : Ukicheza na mtu mwenye Ukimwi, wewe pia utakushika. Ukiogelea pamooja na mtu mwenye Ukimwi, nawe Ukimwi utakupata. Ukila pamoja na mtu mwenye Ukimwi, nawe utakupata. Usieneze uwongo, Machati! Huwezi kupata Ukimwi kwa kusalimiana, kwa kucheza pamoja, kwa kuogelea pamoja au kula pamoja na mtu mwenye Ukimwi.

<원문출처 : Marshal, Mchangamwe, Aboud B. & Jamaadar, A., Msingi wa Kiswahili 2: Darasa la Pili (Nairobi, Longhorn Publishers Ltd., 2003). ), p. 102.>

 

9) 1.8 감정의 표현

 

Mkude : Aika, mbona umenuna?

Aika : Kwa sababu umempa Dora viatu vipya kwa kuwa viatu vyake vimepasuka lakini mimi hujanipa chochote ingawa saa yangu imeharibika.

Mkude : Samahani Aika, nilikuwa nimesahau. Na wewe nimeshakununulia saa. Hii hapa.

Aika : Asante sana. Sasa nimefurahi.

Mkude : Niliamua kukununulia saa mpya kwa kuwa nilikuona huna saa, kwani saa yako haitengenezeki.

Aika : Asante sana.

<원문출처 : Marshal, C. et. al., Sema Kiswahili : Furahia Tanzania, Version Two, A Kiswahili course for peace Corps Tanzania (Arusha, Peace Corps Tanzania, 1998), p. 111.>

 

음쿠데 : 아이카, 왜 시무룩하니?

아이카 : 왜냐하면 네가 도라(Dora)에게는 그녀의 구두가 찢어졌다는 이유로 새로운 구두를 사 주었지만 나에게는 아무것도 주지 않았기 때문이야, 내 시계가 망가졌는데도 말이지.

음쿠데 : 미안해 아이카(Aika), 내가 기억하지 못했어. 너를 주려고 시계를 사왔어. 여기 있어.

아이카 : 정말 고마워. 지금 나는 기쁘다.

음쿠데 : 너에게 새 시계를 사줘야겠다는 결론에 이르렀어. 왜냐하면 너는 시계를 가지고 있지 않고 너의 시계가 고칠 수 없기 때문이야.

아이카 : 정말 고마워.

<관련어휘>

amua : v. 논쟁을 끝마치다, 결론에 이르다, 중재하다.

chukia : v. 화나다. 다른 사람을 미워하다.

fadhaika : v. 당황해하다, 의기소침해 하다.

furaha(-) : 기쁨, 즐거움, 행복.

furahi : v. 기뻐하다, 기쁘다, 즐기다

furahi : v. 기쁘다.

haribika : v. 거칠다, 황폐하다, (음식이) 썩다.

hisia(-) : 감정, 느낌.

huzunika : v. 슬프다.

ingawa : conj. 가령 ~일지라도.  

kasirika : v. 화나다.

kiatu(vi-) : 샌들, 구두.  

kwa kuwa : 왜냐하면.

kwa sababu : 왜냐하면.

kwani : conj. 왜?, 왜냐하면, ~때문에.

lakini : conj. 그러나, 그럼에도 불구하고.

mbona : interrog. 왜? cf.) kwa nini : 왜?

mwizi(wezi) : 도둑.

nuna : v. 실쭉거리다, 골나다, 시무룩하다, 뾰로통하다, 못마땅해 하다, 불친절하다.

nunua : v. 사다.

ona : v. 보다, 느끼다, 생각하다, 믿다, 인정하다.

pa : v. 1.주다 2. 실행하다, 실천하다, 완성하다.  

pasua : v. 1.찢다, 조각내다. 2.자르다. 3.수술하다.

pitika : 유통될 수 있다, 통과될 수 있다.  

pya : adj. 새로운, 신선한, 현대의.  

saa(-) : 1.시간, 기간. 2.시계.

sahau : v. 잊다, 기억하지 못하다, 부주의하다.

sahau : v. 잊다.

sasa : adv. 지금, 현재, 요즈음.  

shangaa : v. 놀라다.

sikitika : v. 유감이다, 슬프다.

stuka / shtuka : v. 충격을 받다.

tengenea : v. 1.정리되다. 2.사용할 수 있다. 3.규칙적이다.

tengeneza : v. 1.정돈하다, 고치다, 수선하다. 2.해결하다, 결정하다.  

tengenezeka : v. 수리되다.

tulia : 조용하다, 냉정하다.

udhika : 괴롭히다, 성가시게 하다.

ugua : v. 아프다, 병나다.

나. 2. 구문연습

1) 2.1 Wanyama wanaofugwa

Mimi ninaishi Arusha. Rafiki zangu Jose na Iguna wanaishi Kiteto. Nyumbani kwao kuna ng'ombe, mbuzi na kondoo. Wote hao ni wanyama wanaofugwa nyumbani. Hawaishi porini.

Ng'ombe ni mkubwa. Miguu yake ni mirefu. Ana nguvu sana. Anaweza kumsukuma mtu akaanguka chini. Ng'ombe hula majani. Akishiba hulala chini. Anacheua majani na kuyatafuna tena. Jose na Iguna hukamua maziwa ya ng'ombe. Maziwa hayo hutumika kupikia chai. Chai ya maziwa ni tamu sana.

Iguna anapenda kuchunga mbuzi. Mbuzi ni wajanja sana. Wanaruka ruka na kukimbia porini. Wanapigana vichwa. Wanapenda kupanda juu ya mawe. Iguna na Jose watachinja mbuzi siku ya sikukuu. Nyama ya mbuzi ni tamu sana.

Kondoo wanafanana na mbuzi, lakini ni wanene. Kondoo wengine wana mikia minene sana. Wakitembea mkia hujipiga upande huu na ule. Kondoo wana manyoya mengi. Kisha wao ni wapole, sio wakorofi. Hawapigi kelele ovyo. Wanatembea kwa pamoja.

Kondoo wanalia baa! baa! Iguna anachunga kondoo. Anapenda kuona kondoo wakipigana. Wanarudi kinyume nyume halafu wanagongana vichwa kwa nguvu. Inatisha sana. Mimi na Jose hatupendi gomvi. Tukiona wanapigana tunawafukuza.

<원문출처 : Mbilinyi, Dorothy A.S., Kiswahili: Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Ben and Company Ltd., 2002), pp. 52-54.>

 

2) 2.2 Hospitali

 

Wanafunzi wote wa darasa la kwanza jana tulikwenda hospitali. Tulikwenda kupimwa macho na masikio. Zakia alipopimwa akaambiwa jicho lake moja ni bovu. Mganga akampa dawa. Akamwambia asicheze kwenye vumbi.

Baadaye tukapimwa masikio. Joni na Hamida wakaambiwa masikio yao ni mabovu.

Mganga akatoa uchafu mwingi. Kisha akawaweka dawa masikioni. Mwisho akasemA :  Kila siku msafishe macho na mutunze masikio yenu vizuri.

<원문출처 : Masoud, A., Kiswahili: Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Oxford University Press Tanzania, 2002), pp. 39-40.>

 

3) 2.3 Nzi

 

Nzi ni mduduu mchafu sana. Anapenda kueneza uchafu. Analeta ugonjwa wa kipindupindu. Hakuna mtu anayempenda nzi. Mwalimu anasema :  Nzi ni adui yetu. Tuoshe matunda kabla ya kula. Tuchemshe maji ya kunywa. Tunawe mikono yetu kwa sabuni baada ya kutoka chooni.

<원문출처 : Masoud, A., Kiswahili: Darasa la Kwanza :  Kitabu cha Mwanafunzi (Dar es Salaam, Oxford University Press Tanzania, 2002), p. 44.>

 

4) 2.4 Afya na usafi

Nuna anatia vidole mdomoni na puani.

Nuna anakohoa. Anawaelekea wenzake. Hafuniki mdomo wake.

Nuna anaomba peremende kutoka mdomoni mwa Juma.

Sufu anaokota sindano na nyembe kutoka pipa la taka. Sufu ana jeraha mguuni. Jeraha linatoka damu. Sufu hakufunga bendeji. Anacheza mpira.

<원문출처 : Mchangamwe, Aboud B., Msingi wa Kiswahili: Darasa la Kwanza (Nairobi, Longhorn Publishers Ltd., 2003), pp. 96, 104.>

 

5) 2.5 Historia ya Afrika Kusini122)

6)

●Kuanza kwa zama za ukoloni.

Kadri mji wa Cape yalivyozidi kukua kutoka kuwa kituo cha makutano hadi kuwa koloni katika karne ya 17, ndivyo upinzani wa Khoikhoi dhidi ya juhudi za wakoloni za kunyakua ardhi ya mababu ulivyoongezeka.

Wakichochewa na watumwa kutoka ukanda wa Mashariki, wakoloni walienea hadi katikati wakijihusisha na shughuli za kilimo huku wakizungumza lugha yao ya Kiafrikana, ambayo ilianzia Cape kutokana na mizizi ya Kidachi. Bila kizuizi, mfumo wa kijamii wa kibaguzi ulichipua kati ya wakoloni na watu weusi wa maeneo ya bara. Mwaka 1779, kushindania maeneo ya malisho kulisababisha kuzuka kwa vita ya kwanza kati ya tisa vilivyopiganwa kati ya watu weupe na Waxhosa, katika eneo la Mashariki ya Cape.

Mwaka 1795 Jimbo la Cape liliunganishwa katika utawala wa Kiingereza, lakini miaka minane baadae lilirejeshwa tena kuwa Jamhuri ya Batavia, jina jipya la Uholanzi chini ya utawala wa Napolioni. Mwaka 1806, Jimbo hili lilichukuliwa tena na utawala wa mabavu wa Uingereza. Hata hivyo, ongezeko jipya la masetla wa Kiingereza mwaka 1820, lilisababisha wapigania uhuru wa kisiasa, pamoja na mambo mengine, kuendesha kampeni kudai uhuru wa kujieleza.

Ikiguswa na hali ya ukosefu wa utulivu katika ukanda wa Mashariki ya Cape, Serikali ya Kikoloni iliingiza nchini masetla wengi zaidi, jambo lililoimarisha zaidi uzalendo wa Makaburu. Vurugu za mipakani ziliendelea kukiwa na mashambulizi kuzunguka Mto Keiskamma mwaka 1834, lakini hatimaye Waxhosa 12,000 walirudishwa nyuma na majeshi ya Waingereza. Kufikia wakati huu, masetla wa Kiafrikana walikuwa wamesonga mbele zaidi kuelekea Mashariki na kuanzisha kambi katika eneo la Port Natal, ambapo baadae paliitwa Durban. Kuanzia mwaka 1838 hadi 1843, walitawala jamhuri yao wenyewe ya Natalia lakini mwaka 1843 Natal ilifanywa tena kuwa koloni la Waingereza. Mwaka 1854, serikali wakilishi isiyo ya kibaguzi iliundwa katika Koloni la Cape ikifuatiwa na ya Natal mwaka 1956.

 

●Kuongezeka kwa Migogoro

Kufikia katikati ya miaka ya 1800, Waafrikana walikuwa wameshaishi katika Jimbo la Cape kwa takribani miaka 200. Waliendelea kupinga utawala wa Waingereza na walichukizwa na mkataba wa uhuru wa Wakhoikhoi na kufutwa kwa biashara ya watumwa mwaka 1834. Mwaka huohuo, uhamaji mkubwa—Great Trek—wa Waafrikana kuelekea Kaskazini ulianza.

Wahamaji masetla wa Kiafrikana na Kiingereza kwa pamoja walikuwa wakimbizi wa vita ya Mfekane, amabayo ilikuwa ni mfululizo wa mapinduzi ya umwagaji damu ya kikabila ambapo mfalme Shaka aliunda taifa moja la Kizulu kutokana na falme mbalimbali. Wahamaji waliingia katika mzozo na mrithi wa mfalme Shaka, ambaye alikuwa ni Dingane, katika Mto wa Damu (Blood River) mwaka 1879, kabla, baadae mwaka huohuo, kuiangamiza Cetshwayo katika eneo la Ulundi.

Baada ya kusukumwa kuelekea Kaskazini kuvuka Mto Orange na Mashariki katika maeneo ya Drakensberg hadi Natal, wahamaji waliruhusiwa na Waingereza kuanzisha Jamhuri mbili huru za Makaburu—Taifa Huru la Orange (sasa Free State) na Transvaal (sasa majimbo manne ya Gauteng, Mpumalanga, Limpopo, na North West—Kaskazini Magharibi).

 

●Kutoka kuwa eneo duni hadi milki ya thamani

Ugunduzi wa almasi katika Cape Mashariki mwaka 1867 na dhahabu katika eneo la Witwatersrand mwaka 1886 kulibadilisha kabisa sura ya Afrika Kusini milele daima. Ghafla, eneo la kikoloni lililopuuzwa likawa milki ya kibepari iliyotamaniwa kutokana na maelfu ya wahamiaji kulibadili eneo la malisho la mashambani kuwa eneo la kiuchumi lenye shughuli mchanganyiko, madini, na viwanda. Jiji la Johannesburg likawa kitovu cha uchumi; na baada ya muda likawa makazi makuu ya jamii za Wayahudi, Wajerumani, Wagiriki, Wareno, na Waitaliano. Ukuaji wa haraka wa miji ya weusi na weupe,na mfumo wa wafanyakazi wanaohamahama ulikuwa ni mambo yaliyokuwa na athari kubwa kwa siasa.

Misuguano kati ya masetla wa Kiingereza (Uitlanders) na mamlaka za Transvaal ilipelekea kuzuka kwa vita ya kwanza ya Angloboer mwaka 1880. Kipigo cha kuabisha katika eneo la Majuba mwaka 1881 kiliilazimisha Uingereza kurejesha upya serikali huru katika Transvaal. Vita ya pili ya Angloboer ilizuka mwaka 1899 baada ya Rais wa Transvaal Paul Kruger na Mwakilishi wa Uingereza katika koloni la Transvaal Lord Milner waliposhindwa kusuluhisha tofauti kati yao kuhusiana na haki za "Uitlanders". Mwaka 1902, jeshi kubwa la Uingereza hatimaye lilifanikiwa kulishinda jeshi la Makaburu lililokuwa likitumia mtindo wa upiganaji wa kikomandoo.

 

●Kuanzishwa kwa muungano wa Afrika Kusini

Kutokana na kuwa na amani, mji wa Vereeniging ulikuwa mwenyeji wa walioshindwa vitani na mwaka 1908, makoloni manne—Cape, Natal, Orange Free State, na Transvaal—yalikutana kuweka msingi wa uanzishaji wa taifa jipya. Machi 31, mwaka 1910, Muungano wa Afrika Kusini, mamlaka huru, ndani ya Himaya ya Uingereza ilizaliwa. Kwa ujumla, makubaliano yaliwaondoa watu weusi waliokuwa wengi na yaliwaondolea haki ya kumiliki ardhi yao. Kutokana na kutoridhishwa na hali hiyo, watu weusi walianzisha Chama cha Kitaifa cha Weusi (the African Natinal Congress—ANC) mwaka 1912.

 

●Sera ya ubaguzi wa rangi yajiimarisha

Katikati ya kipindi cha Muungano na Vita ya Pili ya Dunia, Afrika Kusini iliendeleakuwa taifa la kisasa na la kiviwanda, na kuanza kuweka sheria za ubaguzi wa rangi katika jamii. Fikra za kizalendo za Makaburu zilijiunga na Chama cha Kitaifa (National Party—NP), chama kilichoahidi kulinda lugha ya Kiafrikana, utamaduni na amali za Makaburu, na kutetea uhuru wa kisiasa na kiuchumi dhidi ya Waingereza. Baada ya kuingia madarakani mwaka 1948, chama cha NP kilianza kubuni mfumo mbaya wa utawala ambao ulikuwa wa kiubaguzi wa kijamii na kisiasa, uliojulikana kama "apartheid". Mfumo huu uliamsha upinzani kutoka kwa watu weusi na uhasama wa kimataifa katika kipindi cha baada ya vita.

Baada ya watu weusi 69 kuuawa katika mji wa Sharpeville mwaka 1960 wakati wakiandamana kupinga sheria ya vibali, shutuma za ulimwengu ziliilazimisha Afrika Kusini kujiondoa kutoka katika Jumuiya ya Madola na kuwa Jamhuri mwaka 1961.

 

●Upinzani waongezeka

Baada ya tukio la Sharpeville, Chama cha ANC kilianzisha jeshi la ukombozi, lililojulikana kama Umkhonto weSizwe, na liliendesha kampeni za uasi/hujuma hali iliyopelekea kukamatwa kwa Nelson Mandela na viongozi wengine. Mwaka 1964, Mandela alihukumiwa kifungo cha maisha katika gereza la Kisiwa cha Robben kwa hatia ya uhaini. Chama kilichokuwa kikitumia nguvu cha Kupigania Haki za Weusi cha Robert Sobukwe kilianzisha harakati za uasi zilizochochea hatua madhubuti zaidi za Dola ili kudhibiti upinzani wa watu weusi.  

Mawaziri Wakuu, BJ Vorster na PW Botha walianzisha marekebisho kadhaa huku wakiimarisha zaidi usalama wa ndani lakini uwiano wa madaraka ulianza kuyumba. Upinzani wa wafanyakazi, vikwazo, na msukumo wa uchumi wa kisasa kwa pamoja viliufanya mfumo wa ubaguzi wa rangi kuyumba. Juni 16, mwaka 1976, wanafunzi wa mji wa Soweto waliandamana kupinga kufundishwa kwa lugha ya Kiafrikaana kwenye shule za watu weusi, na wakiunga mkono kampeni ya kuifanya miji—na nchi—isitawalike. Mfululizo wa matangazo ya hali ya hatari haukuweza kuzima harakati hizo.

 

●Kubadilika kwa hali ya mambo

Katika miaka ya 1980, ukombozi wa nchi za Afrika ulifika katika mipaka ya nchi ya Afrika Kusini, baada ya Angola, Msumbiji, na Zimbabwe kupata uhuru. Kufikia mwaka 1990, Vita Baridi ilikoma. Namibia ilipata uhuru na FW de Klerk alimrithi PW Botha. Mara moja, De Klerk aliondoa marufuku dhidi ya Chama cha ANC, akamwachia huru Mandela, na alianzisha mazungumzo rasmi kuhusiana na kulegeza masuala ya kisiasa. Baada ya majadiliano marefu, yaliyojumuisha vyama kadhaa vya siasa, katiba ya mpito ilikubaliwa na Aprili mwaka 1994, Afrika Kusini ilifanya uchaguzi kwa msingi wa mtu—mmoja, kura—moja kwa mara ya kwanza. Chama cha ANC kilishinda uchaguzi kwa kura nyingi na Nelson Mandela akawa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini tarehe 10 Mei, mwaka 1994.

 

●Nchi ya kidemokrasia

Baada ya uchaguzi, vikwazo vya kimataifa viliondolewa na Afrika Kusini ilirejesha nafasi yake katika mashirika ya kimataifa na kikanda. Rais Mandela alitia saini katiba ya mwisho kuwa sheria tarehe 10 Desemba, mwaka 1996.

Uchaguzi mkuu wa pili wa kidemokrasia uliofanyika Juni mwaka 1999, ulikirejesha madarakani Chama cha ANC. Nelson Mandela alistaafu kutoka katika nafasi ya urais na kumwachia uongozi wa nchi Thabo Mbeki mnamo Juni 16, mwaka Mbeki alikiongoza Chama cha ANC hadi katika uchaguzi mkuu mwingine wa mwaka 2004, ambapo Chama cha ANC kilishinda tena. Katika uchaguzi huu, Chama cha ANC kilipata ushindi wa zaidi ya robo tatu ya viti vyote katika bunge la taifa.

 

●Kinara barani Afrika

Chini ya uongozi wa Mbeki, Afrika Kusini imekuwa mstari wa mbele katika harakati za kusuluhisha migogoro ya muda mrefu katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara,na kuhimiza demokrasia na maendeleo barani Afrika, hususani kupitia Ushirikiano Mpya wa Kiuchumi Barani Afrika(NEPAD). Ujumbe muhimu wa nchi hii kwa ulimwenguni kwamba pamoja na tofauti za rangi ya ngozi ya watu, utengamano wa kisiasa hupatikana kwa njia ya mashauriano na maridhiano.

7) 2.6 Fasihi ya Afrika

Fasihi ya Afrika ni somo linalopendeza kutokana na mapana yake. Ni Jambo linalohusisha maisha ya Waafrika kama njia ya kuhifadhi tamaduni zao kutoka jamii moja hadi nyingine kupitia njia mbalimbali za fasihi ya Afrika. Njia hizi ni kama vile nyimbo, mashairi, hadithi, vitendawili, methali na nahau. Zote zinafanana kwa kuwa hutimiza jukumu moja la kuhifadhi hitoria ya familia kupitia kwa wazee, tabia za Waafrika na kueneza busara kati ya jamii za Waafrika. Njia hizi za fasihi hutumiwa katika tamaduni za Waafrika kama vile kuabudiwa kwa miungu, njia za kukua za Kiafrika kama vile kutahiriwa, miradi ya kujiburudisha na katika kusimuliana hadithi mbalimbali zinazosimuliwa wakati wa jioni katika jamii ya Kiafrika.

Waandishi wa fasihi ya Kiafrika huhusisha miktadha inayoambatana, ingawa si kikamilifu, na ukoloni katika Afrika na jinsi ilivyoathiri tamaduni za Kiafrika kama vile ukoloni wa Ufaransa na ule wa wazungu katika Afrika Kusini. Hawajaendelea sana katika maandishi yao kwa kuwa waandishi wa Marekani na nchi nyingine za magharibi wanajulikana sana kushinda hawa Waafrika na kuzuia maendeleo katika uandishi wa fasihi ya Kiafrika. Kukosekana kwa misingi imara katika siasa za Afrika ni jambo lingine ambalo limezuia waandishi wa Afrika kuendelea kwa sababu viongozi katika Afrika hutumia njia zilezile za ukoloni ambazo ni za ufisadi na za kibeberu na kuweka waandishi katika mazingira mabaya ya kutupwa magerezani ama kuuawa.

Ingawa kuna hizi shida zinazowakumba waandishi wa Afrika, waandishi wengine wamesimama imara katika Magharibi na Mashariki mwa Afrika na wanaendelea kufaulu katika maandishi ya  Kiafrika. Wanaandika maandishi yao kwa lugha za Kiafrika kama njia ya kutoa ukoloni katika bongo za Waafrika  uliopandwa na wakoloni. Hata kama wanajitahidi kufanya hivi, kadri siku zinavyosonga, fasihi ya Afrika  inatupa ule utamu wake kwakuwa inabadilishwa mara kwa mara kulingana na wanaoshuhudia fasihi ile. Kwa mfano, hadithi husimuliwa kwa uzito mkubwa kwa wanaume lakini si kwa wanawake. Kutokana na hali hii, wote wawili husimuliwa hadithi moja lakini huelewa tofauti.

<원문출처 : 아래의 내용을 요약하여 스와힐리어로 번역하였음. Gordon, April. A. & Gordon, Donald. L., Understanding Contemporary Africa (Boulder & London, Lynne Rienner Publishers, 2006), pp. 351-396(African Literature).

 

 

다. 3. 문법

1) 3.1 연결어 a의 용법

연결사 a는 명사와 명사를 연결해주는 기능을 한다.

(1)

(2) Mfano)

(3) sambusa za mboga : 야채 / 채소의 사모사, 야채 / 채소로 만든 사모사

(4) kitabu cha mwalimu : 선생님의 책

 

연결어 a를 이용하여 형용사 구를 만들 수 있으며 또한 동사의 부정형을 연결어 a로 연결하여 형용사구를 만들 수 있다.

 

(5) Mfano)

(6) sufuria ya kufaa : 적당한 그릇(수프리아라는 요리용 솥)

(7) kuni za kutosha : 충분한 장작, 땔감

동사의 전치사 형태들은 어떤 용도나 목적을 드러내기 위해 연결사 a와 함께 사용된다.

Mfano)

kasha la kuwekea nguo : 옷상자(옷을 넣기 위한 상자)

kikapu cha kutilia matunda : 과일 바구니(과일을 담기 위한 바구니)

 

2) 3.2 때를 나타내는 po의 용법

 

스와힐리어에서 때를 나타내는 의문사는 ‘lini(언제)’로 lini는 의문문에서만 사용된다. 평서문에서는 lini 대신에 시간 관계사 'po'를 사용한다. 시제와 어근 사이(목적격 접사가 사용되면 시제와 목적격 접사 사이)에 po를 넣어 ‘때(When)'를 나타낸다. 이런 절은 ’wakati(때, 시간)‘을 나타내는 단어로 시작된다.

 

(1) Mfano)

(2) Kila mahali Tulipokwenda……. : 우리가 갔던 모든 장소.(특별한 장소를 언급하고 있음)

(3) Kila tulipoikwenda……. :  우리가 갔던 모든 곳. 

(4) Kila tuendako. : 우리가 가는 모든 곳

(5) Tulipokwenda. : 우리가 갔을 때

(6) Kila aliposema. : 그가 말했을 때마다

(7) Kila watakapo. : 그들이 원할 때마다

(8) Kila mara aliposema. : 그가 말했을 때마다

(9) Kila asemalo. : 그가 말할 때마다

(10) Tulipoenda Arusha tulijifunza Kiswahili. : 우리가 아루샤로 갔을 때, 우리는 스와힐리어를 배웠다.

(11) Ninapozungumza Kiswahili ninafurahi. : 내가 스와힐리어를 말할 때, 나는 기쁘다.

(12) Atakapofika Moshi, atakunywa bia. : 그가 모시에 도착하면, 그는 맥주를 마실 것이다.

(13) (Wakati) alipokuja sikuwapo. : 그가 왔을 때, 나는 여기에 없었다.

(14) Wanawake walipokwenda msituni walikata kuni nyingi. : 여자들이 숲에 갔을 때 그녀들은 많은 땔감을 베었다.

(15) Anapopika kisamvu anatia chumvi nyingi sana. : 그녀가 키사무(kisamu : 야채요리)를 요리할 때 그녀는 많은 소금을 넣었다.

(16) Tutakapokwenda Nairobi tutamwona rafiki yetu. :  우리가 나이로비에 갈 때 우리는 우리의 친구를 만날 것이다.

 

영어 문장에서 사용되는 ‘때(when)'를 나타내는 절을 만들 때 사용하는 스와힐리어의 부사적 기능 po는 오직 na, li, ta 시제에서만 사용된다. 그러나 미래시제에서는 ta가 아니라 taka로 사용되는데 유의한다.

(17)

(18) Mfano)

(19) Nitakuja. : 나는 올 것이다.

(20) Nitakapokuja……. : 내가 올 때…….

 

만약 목적격 전철이 쓰이면 어순은 주격접사+시제+po+목적격 접사+동사이다.

(21)

(22) Mfano)

(23) Nilipowaona niliwapa magazeti. : 내가 그들을 봤을 때 나는 그들에게 신문을 주었다.

 

po가 단음절동사와 함께 사용되면 부정사 ku를 붙인다.

(24)

(25) Mfano)

(26) Alipokuja alinipa korosho. : 그가 왔을 때 그는 나에게 캐슈열매를 주었다.

(27) cf.) korosho(ma-) : 캐슈열매

3) 3.3 목적어를 가진 명령법

 

목적어가 사용되어 명령법을 사용할 때는 가상법을 사용한다.

 

(1) Mfano)

(2) Pika chakula! : 음식을 요리해라!(Cook some food!)

(3) Kipike! : 그것을 요리해라(Cook it!)

(4) Pikeni chakula! : 약간의 음식을 요리해라!(복수형) (Cook(pl.) some food!)

(5) Kipikeni! : 그것을 요리해라!(복수형) (Cook(pl.) it!)

(6) Uliza swali! : 질문을 해라!(Ask the question!)

(7) Mwulize Juma swali! : 주마(Juma)에게 질문을 하여라!(Ask Juma the question!)

4) 3.4 Ndiyo와 부정적인 질문에 대한 답

 

부정적인 형태의 질문에 대한 답이 ndiyo가 될 경우 ‘예(yes)'로 해석되나 더 정확하게 ‘그래(it is so)’정도로 해석되는데 이러한 대답은 그 질문의 부정을 확인하고 또한 긍정적인 질문을 더욱 확고히 하는 역할을 한다. 아래 문장에서 보이는 부정인 ‘hapana(아니요, no, there is not)’의 기능은 영어에는 없다.

 

(1) Mfano)

(2) A : Je huelewi swali langu? : 당신은 나의 질문을 이해하지 못합니까?

(3) B : Ndiyo, sielewi. : 예, 나는 이해하지 못합니다.

(4) A : Umeelewa swali? : 당신은 그 질문을 이해하십니까?

(5) B : Ndiyo, nimeelewa. : 예, 나는 그것을 이해합니다.

(6) A : Je, husomi Kiarabu? : 당신은 아랍어를 공부하지 않습니까?

(7) B : Hapana, sisomi. : 예, 나는 공부하지 않습니다.

(8) A : Amesoma Kiarabu? : 그가 아랍어를 공부 했습니까?

(9) B : Hapana, hajasoma. : 아니오, 그녀는 아직 하지 않았습니다.

(10)

5) 3.5 질병에 대한 표현

 

ugonjwa는 특정 질병을 언급할 때는 질병의 이름과 함께 사용된다.

(1)

(2) Mfano)

(3) gonjwa : adj. 병이 있는, 좋지 않은, 하기 싫은.

(4) mgonjwa(wa-) : 병자.

(5) ugonjwa(mjagonjwa)123) : 병, 질병.

(6) ugonjwa wa kipindupindu : 콜레라

(7) ugonjwa wa malaria : 말라리아

(8) ugonjwa wa ukimwi : 에이즈

 

그러나 만약 질병들에 대해 하나하나 그 질병이 무엇인지 열거하지 않고 언급하고 싶다면 magonjwa를 사용한다.

(9)

(10) Mfano)

(11) magonjwa ya mzee. : 노인의 병

(12) magonjwa ya nchi za kaskazini. : 북쪽에 있는 나라들의 질병들.

 

‘얻다.’ ‘획득하다.’라는 뜻을 가지고 있는 동사 pata의 수동형은 어떤 사람이 질병에 걸렸음을 가리킬 때 가장 자주 쓰이는 말이다. 이와 같은 뜻을 가진 동사로는 ‘잡다.’ ‘쥐다.’라는 뜻을 가진 shika가 있다.

(13)

(14) Mfano)

(15) Amepatwa na kichefuchefu. : 그는 뱃멀미를 했다.

(16) Mtoto wake Juma amepatwa na homa. : 주마(Juma)의 아이는 고열에 걸렸다.

(17) Bahati mbaya wachezaji wawili wameshikwa na malaria. : 불행하게도 두 선수는 말라리아에 걸렸다.

(18) Siku zile wengi walipatwa na kipindupindu. : 그 당시 많은 사람들이 콜레라에 감염되었다.

(19) Kwa kuwa mtoto anahara wamempelekea zahanati. : 아이가 설사에 걸렸기에 그들은 아이를 병원으로 데리고 갔다.

(20) cf.) hara : v. 설사를 하다. cf.) -hara damu : 피가 섞인 설사를 하다.

6) 3.6 ‘고통’이나 ‘아픔’에 대한 표현

 

아래의 예문 중 첫 번째 문장은 일반적으로 몸의 어느 부위가 아프다는 사실을 표현할 때 쓰는 방법이지만 두 번째 문장은 ‘머리(kichwa)’라는 몸의 특정 부위를 문장의 앞에 주어로 표현함으로서 강조나 주의를 집중시키고 있다. 이 문장의 특징은 누구의 머리인지는 언급할 필요가 없지만 대신 고통을 느끼는 대상을 가리키는 목적격 접사를 반드시 사용해야 한다는 것이다.

 

(1) Mfano)

(2) Anaumwa kichwa. 그는 머리가 아프다.

(3) Kichwa kinamwuma. : 머리가 아프다. / 머리가 그를 아프게 한다.

(4) Mikono unaniuma. : 내 손을 다쳤어요.

(5) Miguu inakuuma? : 너의 발 / 다리가 아프니?

(6) Mgongo unamwuma.: 그의 등이 아프다

(7) Bega linaniuma : 내 어깨가 아파요

(8) Damu inamtoka kichwani. : 그는 머리에서 피를 흘리고 있다

(9) Damu inamtoka. : 그는 피를 흘리고 있다.

(10) Anatoka damu puani. : 그의 코에서 피가 난다.

(11) Anatoka damu. : 그는 피를 흘리고 있다.

 

다음 예문은 신체부위를 가리키는 단어가 끝에 붙어있으며 사람을 가리키는 목적격 접사를 사용하고 있다. 목적격 접사는 ji로 주어와 목적어가 같은 사람을 가리키고 있다. 이 문장을 직역하면 ‘너의 손에 관하여 너 자신(ji)을 칼로 베지 마라.’

(12)

(13) Mfano)

(14) Usijikate mkono. : 너의 손을 칼로 베지 마라.

주어와 목적어가 같지 않은 예문들을 살펴보자

(15) Mfano)

(16) Usimkate mkono. : 그의 손을 베지 마세요.

(17) Asimkate kichwa. : 그녀가 그의 손을 베게 하지 마세요.

(18) Nisimkate kidole. : 내가 그의 손가락을 베게 하지 말아줘.

라. 4. 단어 및 어휘 정리

 

amua : v. 논쟁을 끝마치다, 결론에 이르다, 중재하다.

bado : adv. 아직도, 여전히.

bandeji / gongo(ma-) : 붕대.

basi : cong. 1.(문장 첫머리에서) 자, 그때, 그래서, 그러므로, 그리고 나서 등. 2. (감동사로서) 일반적으로 동의, 수용을 표시한다. 그것으로 되었다. 알았다. 좋다 등. 3.(명령, 결정의 뜻) 거기까지! 이만 끝! 그만 두어라! 등 cf.) Basi twende! : 자아, 나가자!

bega(ma-) : 어깨부분, 견부

chachi / shashi : 가제, (얇고 흰) 옥양목. cf.) karatasi ya shashi : 화장지.

cheua : v. 되새김하다, 트림하다.

chubuko(ma-) : 타박상, 좌상(挫傷).

chukia : v. 화나다. 다른 사람을 미워하다.

daktari(ma-) / mganga(wa-) / tabibu(ma-) / ntabibu(ma-) : 의사

damu(-) : 혈액, 피.

dawa(-, ma-) : 약, 치료.

ependiks : 맹장염.

fadhaika : v. 당황해하다, 의기소침해 하다.

fuga : v. (가축을) 기르다, 키우다.

furaha(-) : 기쁨, 즐거움, 행복.

furahi : v. 기뻐하다, 기쁘다, 즐기다

gari la wagonjwa : 구급차, 앰블런스.

haribika : v. 거칠다, 황폐하다, (음식이) 썩다.

hebu : interj. 여보세요! 잠깐! cf.) Hebu njoo! : 야, 잠깐 오너라!

hisia(-) : 감정, 느낌.

homa ya mafua : 유행성 감기.

homa ya manjano : 황열.

homa(-) : 열병.

hospitali ndogo / zahanati(-) / dispensari(-) / kliniki(-) : 의무실, 진료소, 보건소.

hospitali(-) : 병원.

huduma ya kwanza / msaada wa kwanza : 응급조치, 긴급처치. cf.) huduma / hoduma(-) : 봉사, 친절, 배려, 도움, 고용.

huzunika : v. 슬프다.

ingawa : conj. 가령 ~일지라도.  

jana : 1.(-)과거, 이전. 2.adv. 어제.

jeraha(ma-) : 부상.

kabisa : adv. 1. 완전히, 전체적으로, 모두. 2. 아주, 대단히, 극히. 3. 완벽하게, 정확히.

kamua : v. 짜다.

kasirika : v. 화나다.

kiatu(vi-) : 샌들, 구두.  

kichefuchefu : sing. 구역질, 매스꺼움.

kichocho(vi-) : 주혈흡충증.

kichwa(vi-) : 1.머리, 앞, 사물의 처음 ; 자랑, 거만함. 2. 윗부분, 주요 부분. 3. 주요 인물, 지도자. 4. adv. kichwa kichwa : 무모하게, 앞뒤를 가리지 않고. 5. 두통.

kidole cha mkono : 손가락. kidole(vi-) : 손가락, 발가락.

kidole gumba : 엄지 손가락. cf.) gumba : adj. 1. 고독한, 고립된. 2. 아이가 없는, 불임의.

kijidudu(vi-) : 미생물, 세균, 작은 벌레.

kipindupindu : 콜레라.

kisonono / kisunono(vi-) : 임질. cf.) kisonono cha damu : 주혈흡충증.

kitanda cha wagonjwa / machela(-) : 1. 들것. 2. 해먹.

kitanda(vi-) : 침대.

kiungo(vi-) / kifungdo(vi-) : 관절.

kivi / kiko(vi-) : 팔꿈치.

kiwiko cha mguu : 발목. cf.) kiwiko(vi-) : 손목, 발목.

kizunguzungu : sing. 현기증, 어질어질 함, 편찮음.

kobole(vi-) : 맹장(盲腸).

kope(ma-) : 눈꺼풀.

kozi(-) : 1. 코코넛의 섬유질, 2. 진로, 진행.

kuhara / harisho(ma-) / choo cha majimaji : 설사.  cf.) hara : 1.v. 변이 잘 통하게 하다, 설사하다. -hara damu : 이질에 걸리다. 2. (-) : (도시의) 지역, 지구.

kunywa : v. 마시다.

kupigwa wa jua : 일사병.

kuta : v. 생기다, 일어나다, 우연히 만나다, 알게 되다.

kutoka damu : 출혈.

kuunguza : 화상. cf.) ungua : v. 타다, 겉을 태우다. unguza : v. 그슬리다, 타게 하다.

kuwa : conj. 1. ya kuwa : ~하기 위하여, ~할 목적으로. 2. kwa kuwa : 왜냐하면. 3. v. 1. ~이다. 4. kuwa na : ~을 갖는다.

kuzimia : 기절. cf.) zimia : v. 기절하다, 까무라치다.

kwa kuwa : 왜냐하면.

kwa sababu : 왜냐하면.

kwani : conj. 왜?, 왜냐하면, ~때문에.

lakini : conj. 그러나, 그럼에도 불구하고.

lala : v. 눕다, 자다.

malale(-) / ugonjwa wakusinzia ugonjwa wa malale : 수면병. cf.) malale(-) : 수면병, 뇌염.

malaria(-) : 말라리아. cf.) homa ya malaria : 말라리아 열.

matako : pl. 엉덩이, 둔부.

matibabu : pl. 치료, 진료.

maumivu ya kichwa : 두통. cf.) umivu(maumivu) : 고통, 통증, 아픔, 쓰림.

mbona : interrog. 왜? cf.) kwa nini : 왜?

mfupa(m-) : 뼈.

mgonjwa(wa-) : 환자.

mguu(mi-) : 다리.

moyo(mioyo) : 심장, 마음.

mpaka sasa : 지금까지.

Msalaba Mwekundu. : 적십자(赤十字).

mshipa wa damu : 혈관. cf.) mshipa(mi-) : 1. 정맥, 동맥. 2. 맥박. 3. 신경, 근육, 힘줄.

mshtuko / mstuko(mi-) : 1. 갑작스럽게 놀람, 발작. 2. 충격, 타격. 3. 삠, 겹질림. cf.) mshtuko wa ubongo : 졸도.

mvunjiko wa mfupa : 골절.

mwili(miili) : 1.(인간 혹은 동물의) 신체. 2. 머리를 제외한 몸통. 3. fig. 비행, (비행기의) 동체, 기체.

mwizi(wezi) : 도둑.

mwuguzi(wa-) : 간호원.

mzio(-) / wenga(-) : 알레르기

na : 1.(접속사로서) 그리고, ~과. 2.(전치사로서) ~와, ~으로, ~와 더불어, ~로부터.  3.(동사로서) 가지고 있다.

nena(ma-) : 겨드랑이.

ngoja : v. 기다리다.

nguvu(-) : 1. 힘, 원기, 권력, 에너지. 2.권력, 능력, 영향력. 3. 중요성, 진지함. 4. 정렬, 격렬함, 맹렬함, 열성. cf.) kwa nguvu : 1. 힘차게, 강하게, 진지하게, 2, 강제로, 강압적으로, 마지못해서.

nini : interrog. pron. 무엇?

nuna : v. 실쭉거리다, 골나다, 시무룩하다, 뾰로통하다, 못마땅해 하다, 불친절하다.

nunua : v. 사다.

nyumba(-) : 집.

ona : v. 보다, 느끼다, 생각하다, 믿다, 인정하다.

pa : v. 1.주다 2. 실행하다, 실천하다, 완성하다.

paji(ma-) : 1. 선물. 2. 희생, 희생물. 3. 이마. cf.) paji la uso : 이마.

pasua : v. 1.찢다, 조각내다. 2.자르다. 3.수술하다.

peleke : v. 데려가다, 인도하다.

picha ya eksrei : 엑스레이 사진.

pima : v. 1. 재다, 측정하다. 2. 비판적으로 고려하다, 평가하다, 비판하다. cf.) -pima upana : 넓이를 재다. -pima halijoto la mwili : 체온을 재다. Halijoto ya kawaida ya mwili wa binadamu ni nyuzi joto 36.9'. : 일반적으로 사람의 몸의 온도는 36.9도이다. cf.) Alipimwa na kuonekana na vijidudu vyaaa Ukimwi. : 그는 HIV에 걸린 것으로 반응하였다.

pitika : 유통될 수 있다, 통과될 수 있다.  

pya : adj. 새로운, 신선한, 현대의.  

risiti(-) / cheti(vy-) : 처방. cf.) risiti(-) : 수령, 수취.

saa(-) : 1.시간, 기간. 2.시계.

sahau : v. 잊다, 기억하지 못하다, 부주의하다.

sasa : adv. 지금, 현재, 요즈음.  

shangaa : v. 놀라다.

shauri(ma-) : 1. 계획, 의도, 프로젝트, 안건.  2. 충고, 상담, 의논, 토의. 3. 토론, 논쟁. cf.) -fanya shauri : 고려하다, 의논하다, 기획하다.

shavu(ma-) : 뺨, 볼.

shinda : v. 극복하다, 정복하다.

sikia : v. 1. 느끼다, 인지하다, 알다. 2. 듣다.

sikitika : v. 유감이다, 슬프다.

simama : v. 일어서다.

sindano(-) : 바늘, 주사.

stuka / shtuka : v. 충격을 받다.

sumbua : v. 걱정하다, 고민하다. cf.) sumbuliwa : v. 괴롭힘을 당하다.

tafuna : v. 씹다, 먹다.

tangu : prep. (=taka, kutoka) ~이래로, ~로부터.

tembelea : v. 방문하다. cf.) tembea : v. 걷다, 여행하다.  

tengenea : v. 1. 정리되다. 2. 사용할 수 있다. 3. 규칙적이다.

tengeneza : v. 1. 정돈하다, 고치다, 수선하다. 2.해결하다, 결정하다.

tengenezeka : v. 수리되다.

tetemeka : v. 시시나무 떨듯 떨다. cf.) tetema : v. 떨다, 전율하다, 흔들리다.

tetemeko / tetemo(ma-) : 떨림, 흔들림, 전율, 진동.

tiba / tabibia(-) : 약, 제약, 의약품.

tulia : 조용하다, 냉정하다.

tumbo(-) : 1. 배, 위. 2. 자궁. 3. 위장이나 내장의 통증. 4.fig. 어떤 물건의 내부. 5. 용기, 돌출.

udhika : 괴롭히다, 성가시게 하다.

ugonjwa wa kuambukiza : 전염병. cf.) ambukiza : v. 병을 옮기다, 유행시키다. ambukizo(ma-) : 병의 전염.

ugonjwa wa matumbo : 위염.

ugua : v. 아프다, 병나다.

umedhurika na chakula kibaya : 식중독.

umwa : v. 해를 입다. cf.) uma : v. 물다, 해치다, 아프게 하다.

usiku(siku) : 1.(siku) 밤, 야간(저녁 6시에서 아침 6시까지). 2. adv. 밤에.

utunzaji / utunzi : sing. 간호, 보호, 돌봄.

vipi : interrog. 잘 지내? 어때? 이봐.

vizuri : adv. 좋은

zahanati(-) : 의무실, 의료원.

●에이즈 ukimwi(=ukosefu wa kinga mwilini) : 에이즈. cf.) Pamoja tuangamize ukimwi! : 우리 함께 AIDS를 퇴치하자! angamaa : v. 공중에 떠 있다, 매달려 있다. 저장하다, 비축하다. angamia : v. 파괴하다, 실패하다. angamiza : v. 파괴하다, 철저히 때려눕히다. waya  / ugonjwa wa kisasa : (구어상) 에이즈. vita dhidi ya ukimwi : 에이즈와의 싸움. mtu mwenye virusi vya ukimwi : 에이즈 바이러스 보균자.

●약복용 시간 kila saa : 매시간. baada ya chakula : 식후에, kabla ya chakula : 식전에. unapokwenda kulala : 잠 들 적에. unapoamka : 일어났을 때. mara mbili kila siku : 1일 2회.

●신체부위 jino(meno) : 이, 치아. ulimi(ndimi) : 혀. nyusi(-) : 눈썹. kope(ma-) : 눈꺼풀. ukope(kope) : 속눈썹. kiini(-) : 1. 눈동자. cf.) kiini cha jicho : 눈동자. 2. 안쪽, 내부, 핵, 중심. 3. 본질, 정수. mboni(-) : 1. 눈동자, 동공. 2. 값진 것, 소중한 것. 3. 잃어버린 것 / 사람. jicho(ma-) : 눈. unywele(nywele) : 머리카락. pua(-) : 코. cf.) -piga pua : 코를 풀다. sikio(ma-) : 귀. kinywa / kinwa / kanwa(vi-) : 입. shavu(ma-) : 뺨, 볼. cf.) 놈펴 la uso : 뺨. 놈펴 la mguu : 장딴지. paji(ma-) : 이마. cf.) paji la uso : 이마. taya(ma-) / kitaya(vi-) / utaya(taya) : 턱, 턱뼈. sharubu / shuarub / shuarubu(ma-) : 턱수염, 구레나룻. udevu(ndevu / madevu) : 1. 얼굴에 난 털, 수염. 2. 안테나, 수상기, 곤충의 더듬이.  ufizi(fizii) : 잇몸, 치경. sine(ma-) : 잇몸, 치경. shingo(ma-) : 목. koo(ma-) : 목구멍, 인후(咽喉). bega(ma-) : 어깨. kiuno(vi-) : 허리. tako(ma-) : 엉덩이, 둔부. mkono(mi-) : 손. kidole(vi-) : 손가락. goti(ma-) : 무릎. dhiraa(-) : 완척(腕尺 ; 팔꿈치에서 가운데 손가락 끝, 또는 손바닥까지의 길이. 약 46-50cm). kiwiko(vi-) : 팔꿈치. kwapa(ma-) : 겨드랑이. ngumi(-) : 주먹. kifundo(vi-) : 1. 매듭, 리본 묶음. 2. 관절. cf.) kifundo cha mguu : 발꿈치(발목). kifundo cha mkono : 팔꿈치(팔목). kitanga(vi-) : (작고 둥근 예배용) 돗자리, 기도방석. cf.) kitanga cha mkono : 손바닥. kitanga cha mguu : 발바닥. chanda(vy-) : 손가락, 발가락. ukucha(kucha) : 손톱, 발톱.  3. 술, 장식 술. nguyu(-) : 발목뼈, 복사뼈. wayo(nyayo) : 발자국, 흔적, 발바닥. kisigino / kishigino(vi-) : 발뒤꿈치, 발꿈치.  paja(ma-) : 넓적다리, 허벅지. mguu(mi-) : 다리. kitovu(vi-) : 1. 배꼽. 2. 중앙, 중심. 3. 차의 추축(樞軸). tumbo(ma-) : 배. kifua(vi-) : 가슴. kidevu(vi-) : 턱. cf.) ndevu za kidevu : 염소 수염. mdomo(mi-) : 입술, 입. kichwa(vi-) : 머리. mgongo(mi-) : 등. bongo(ma-) : 뇌. koo(ma-) : 목구멍, 목젓. umio(mio) : 목젓, 후두, moyo(mioyo) : 심장. pafu / bafu(ma-) : 허파. ini(ma-) : 간. figo(ma-) / nso(-) / buki(ma-) : 콩팥. kibofu(vi-) : 방광. mshipa(mi-) : 1. 정맥, 동맥. 2. 맥박. 3. 근육, 힘줄. musuli(mi-) : 근육. fuvu(ma-) : 두개골. cf.) fuvu la kichwa : 두개골. mtulinga(mi-) : 쇄골. ubavu(mbavu) : 갈비뼈. uti(nyuti) : 1. 나무의 통, 줄기. 2. uti wa mgongo : 등뼈. 3. 나무토막, 쪼개진 조각. muundi(miundi) : 정강이뼈,

 

<속담>

●Ajali haina kinga. : 운명은 막을 수 없다.

●La kuvunda halina rubani. : 망가진 배에는 항해사가 필요 없다.

●Kila mlango una ufunguo wake. : 모든 문은 열쇠를 갖고 있다.

●Riziki, kama ajali, huitambui ijapo. : 사람의 섭리라고 하는 것은 운명과 같은 것이다. 언제 그것이 오는지 알 수 없기 때문이다.

●Ukipata bahati mbaya, usiangalie kichoko. : 운이 안 좋았다고 하더라도 아픈 데를 보지 마라.(낙담해서는 안 된다.)

●Waliapo ndipo wachekapo. : 우는 곳에서 또 웃게 될 것이다.(슬픔은 기쁨으로 변한다. 어떤 사람은 깊이 슬퍼하고, 또 어떤 사람은 불운의 중요성 때문에 기뻐한다.)

●Dau la mnyonge haliendi joshi, likienda joshi ni Mungu kupenda. : 가난한 사람의 보트는 바람을 거슬러 항해하지 않는다. 만약 배가 바람이 불어오는 쪽으로 항로를 바꾼다면, 그것은 신이 그렇게 했기 때문이다.

●Kuku wa mkata hatagi, na angetaga haangui, na akiangua halei, na akilea hutwaliwa na mwewe. : 가난한 사람의 암탉은 알을 낳지 못한다. 그리고 암탉이 알을 낳을 지라도 암탉은 결코 부화시키지 못한다. 그리고 부화시킬지라도, 암탉은 결코 병아리를 기를 수 없다. 그리고 암탉이 병아리를 기르면 매가 채어간다.

 

아프리카인들은 운명에 대해 대부분 순응적인 태도를 보인다. 오랜 시간동안 자연의 힘을 경험적으로 터득한 이들은 인간의 힘으로는 어쩔 수 없는 일에 대해서는 긍정적으로 받아들이는 것이 지혜로운 대처방법이라고 생각하는 것이다. 또한 순환적인 자연의 흐름을 통해 생명과 가치를 갖고 있는 것들은 언젠가는 소멸하기 마련이라는 교훈을 간직하고 있다. 이와는 다른 맥락에서 ������모든 문에는 열쇠가 있다������식의 비유를 통해 모든 문제에는 그에 맞는 해결책이 존재하며, 모든 사람에게는 자신의 동반자가 있다는 적극적인 운명의식을 보여주기도 한다.  

32.

33.